Posts

Showing posts from July, 2017

Aishi Manula RASMI SIMBA

Image
Golikipa Aishi Munula ambaye alikuwa anakipiga na klabu ya Azam FC amejiunga rasmi na klabu ya Simba na kesho atakwea pipa kujiunga na klabu hiyo ambayo sasa ipo nchini Afrika Kusini kwa maandalizi za msimu ujao.  Kwa mujibu wa Haji Manara amesema kuwa klabu ya Simba imeshamalizana na mchezaji huyo na kudai ameahidi makubwa kwa mashabiki wa Msimbazi  "Golikipa wa kimataifa wa Tanzania Aishi Salum Manula kesho tarehe moja, anatarajiwa kujiunga rasmi na kambi ya klabu yetu ya Simba iliopo Eden Vale Johannesburg, nchini Afrika kusini. Manula ambaye ameshamalizana kila kitu kuhusu kujiunga na klabu yetu, na ameahidi kuwapa furaha wanachama na washabiki wetu, sambamba na kuisaidia klabu kushinda mataji itakayowania msimu huu" alisema Haji Manara  Mbali na hilo Simba kesho inatarajiwa kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya mabingwa Afrika Orlando Pirates ya nchini Afrika kusini.

Magazetini leo

Image

DOWNLOAD PERFECT KOMBO REMIX kwenye blog yetu

Image
Perfect kombo remix download hapo chini click link hii https://www.jamaaonline.com/files/download/196

MJADALA MZITO simba KUHUSU KUMVUA UKAPTENI mkude

Image
Taarifa za uongozi wa timu ya Simba pamoja na benchi la ufundi chini ya kocha mkuu Joseph Omog kumvua unahodha kiungo wake wa kutumainiwa Jonas Mkude limeendelea kuzua mjadala ambapo nahodha wa zamani wa timu hiyo, Henry Joseph amefunguka. Henry Joseph maarufu kwa jina la 'Shindika' ameongea na gazeti la Mwananchi kutokea nchini Norway ambapo alisema wazi kuwa timu hiyo imefanya jambo lisilo la kiungwana kulinganisha na kazi yake aliyoifanya ndani ya timu hiyo. Shindika alisema kiungo huyo hata kama alikuwa na makosa binafsi lakini sio sababu ya yeye kuvuliwa jumla uongozi huo badala yake ilipaswa angalau apewe unahodha msaidizi ambapo alishauzoea. "Kiukweli mimi sijafurahishwa na uamuzi uliofanywa na timu kumvua unahodha kulingana na kazi kubwa anayoifanya uwanjani lakini pia ingependeza zaidi kama wangemfanya nahodha msaidizi," alisema Shindika. Katika hatua nyingine Nahodha huyo wa zamani wa Taifa Stars mbali na kukumbushia jinsi yeye mwenyewe al

JELA MIAKA 10 KWA kusingizia kubakwa na wanaume watatu

Image
Msichana mkazi wa Texas, Marekani ambaye alikimbilia Kanisani na kudai kuwa amebakwa na kundi la Wanaume watatu wenye asili ya Afrika, huenda akahukumiwa kifungo jela baada ya kukiri kwamba alidanganya.  Breana Harmon, mwenye umri wa miaka 19, mapema mwezi March alikimbilia Kanisani mjini Denison, Texas, akiwa na nusu uchi na mwili wake ukiwa damu na kudai kubakwa na wanaume wawili wakati mwingine akimshikilia chini, unaripoti mtandao wa KXII.  Hata hivyo, vipimo vya Hospitali havikuonesha ushahidi wowote kuwa msichana huyo alidhalilishwa na wanaume hao wenye asili ya Afrika ambapo wiki mbili baada ya tukio hilo alikiri kwa Polisi kuwa alidanganya juu ya tukio hilo na kuumia kwake kulitokana na yeye mwenyewe.  Kwa mujibu wa Mwanasheria Joe Brown, msichana huyo alifunguliwa kesi ya jinai mapema wiki hii kutokana na kudanganya ambapo thamani ya kosa ni kifungo cha hadi miaka 10 jela na faini ya Dollar 10,000.  “Tulivyoangalia katika kilichotokea kwenye kesi hii, na kuzingatia madhar

TAMBWE:Kambi yanga Morogoro ni kama jeshini

Image
Yanga ipo kambini Morogoro ikijiandaa kwa ajili ya msimu ujao, mshambuliaji wa timu hiyo, Amiss Tambwe amezungumza akiwa kambini na kuelezea kinachoendelea. Tambwe amesema kuwa kambi yao ni kama jeshi kwa kuwa mazoezi ni magumu na ni matamu, kwa kuwa anajua ili timu iwe fiti lazima wapate muda wa kujiandaa kama wanavyofanya wao.  Amesema wapo mafichoni huko lakini kila kitu kinaendelea vizuri, pamoja na hivyo ameongeza kuwa atapambana ili kupata nafasi ya kuchukua kiatu cha dhahabu, yaani ufungaji bora.  Ameongeza kuwa anajua msimu ni mgumu lakini atapambana anavyoweza ili kuiwezesha Yangakufanya vizuri licha ya kutambua kuwa msimu utakuwa mgumu.

Hatimaye NEYMAR arejea mazoezini baada ya ugomvi

Image
 Baada ya kuzichapa na beki mpya wa Barcelona, Nelson Semedo , mshambuliaji Mbrazil, Neymar amerejea mazoezini.  Barcelona bado iko Miami nchini Marekani na Neymar alitoka mazoezini kwa hasira baada ya ugomvi huo jana.  Baadaye ikaelezwa hatarejea Hispania na Barcelona na yuko katika mpango wake wa kutaka kuondoka kujiunga na PSG ambayo inamtaka kwa udi na uvumba.  Hata hivyo, leo amerejea mazoezini lakini akionekana ni mtu asiye na furaha. 

Remix perfect kombo

Image
Perfect kombo remix Imekaaje hii mdau wangu

NENO LA OKWI KWA MASHABIKI WAKE

Mshambuliaji wa kimataifa wa Simba kutoka Uganda, Emmanuel Okwi, ametua kambini Afrika Kusini jana na kuwaambia mashabiki wa timu hiyo wajiandae kuona "vitu vyake" katika mechi ya kirafiki dhidi ya Rayon FC itakayofanyika Agosti 8 (Simba Day).  Okwi amewaambia mashabiki na wanachama wa Simba wawe watulivu, amejiandaa kuwapa kile wanachokitarajia kutoka kwake na anafahamu vizuri ndoto za klabu hiyo yenye makao makuu yake Mtaa wa Msimbazi, Kariakoo jijini.  "Nitakuwa Dar es Salaam siku ya Simba Day, najua watu wanahamu ya kuniona, mashabiki wawe watulivu," alisema mshambuliaji huyo.

First Eleven Chelsea VS Inter

Image
Team to face Inter: Courtois; Azpilicueta, David Luiz, Cahill (c); Moses, Kante, Fabregas, Alonso; Willian, Batshuayi, Morata.

MSUVA DEAL DONE morocco

Image
Simon Msuva (katikati) akitambulishwa. ALIYEKUWA winga machachali wa Klabu ya Yanga na Timu ya Taifa ya  Tanzania (Taifa Stars) , Simon Happygod Msuva ametangazwa rasmi kujiunga na Klabu ya  Difaa El Jadida  ya nchini  Morocco kuitumikia timu hiyo . Akiwa klabuni hapo. Msuva  ambaye ni mfungaji bora wa Michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2016/17 amejiunga na klabu hiyo ikiwa ni siku mbili tangu aondoke  Tanzania  kwenda nchini humo kwa ajili ya vipimo vya afya kabla ya kujiunga nayo. Akikabidhiwa jezi. Msuva  amepata nafasi ya kujiunga na  Defaa El Jadida  kwa mkataba wa miaka mitatu na tutamuona katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika akiichezea  El Jadida  ambayo imemaliza msimu ikiwa nafasi ya pili nyuma ya  Wydad Casablanca  kwa tofauti ya point saba. Msuva sasa anaungana na Ramadhani Singano ‘Messi’ aliyekuwa akiichezea Klabu ya Simba na baadaye Azam FC ambaye pia amejiunga na Difaa El Jadida.

OKWI AIFUATA SIMBA SOUTH

Image
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Simba kutoka Uganda, Emmanuel Okwi, ametua kambini Afrika Kusini jana na kuwaambia mashabiki wa timu hiyo wajiandae kuona "vitu vyake" katika mechi ya kirafiki dhidi ya Rayon FC itakayofanyika Agosti 8 mwaka huu (Simba Day) kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Saalam.   Okwi, alisema kuwa mbali na kuchelewa kujiunga na kambi ya timu hiyo, yuko katika kiwango kizuri na benchi la ufundi halitakuwa na kazi kubwa kuinua kiwango chake.  Okwi amewaambia mashabiki na wanachama wa Simba wawe watulivu, amejiandaa kuwapa kile wanachokitarajia kutoka kwake na anafahamu vizuri ndoto za klabu hiyo yenye makao makuu yake Mtaa wa Msimbazi, Kariakoo jijini.  "Ninaenda Sauzi leo (jana), nitakuwa Dar es Salaam siku ya Simba Day, najua watu wanahamu ya kuniona, mashabiki wawe watulivu," alisema kwa kifupi mshambuliaji huyo kutoka SC Villa ambaye anawania kiatu cha dhahabu katika Ligi Kuu ya Uganda.  Nyota wengine wapya ambao wanadaiwa kusajiliwa na Simba

SAFARI YA KICHUYA YATIMIA SASA

Image
Siku chache baada ya kiungo wa Simba, Said Ndemla kwenda Sweden kufanya majaribio katika Klabu ya AFC, mshambuliaji wa timu hiyo, Shiza Kichuya anaweza akapata shavu la kucheza soka nchini Misri.  Taarifa kutoka ndani ya Simba zinasema klabu moja ya Misri inamtaka Kichuya ili imsajili kwa ajili ya kuichezea timu yao na sasa wapo katika mazungumzo.  Bado mazungumzo ya Simba na klabu hiyo yanaendelea na wakifikia muafaka muda wowote Kichuya ataondoka kwenda nchini humo.  “Kuna timu ya Misri kupitia wakala aliyemuona Kichuya kwenye ligi na kufanya mawasiliano na sisi na tayari kuna barua wameleta wakimtaka Kichuya.  “Kuna dau ambalo wamelipendekeza ili waweze kumsajili Kichuya lakini sisi hatujakubaliana nalo, hivyo tupo katika mazungumzo ya kuweza kufikia makubaliano lakini tunataka waongeze dau.  “Hata hivyo, itabidi tumuachie Kichuya akacheze soka la kulipwa kwani kumzuia mchezaji kwa sasa ni sawa na bure, kwani amebakiza mwaka mmoja katika mkataba wake na hatutaki baadaye aende bur

RIHANNA NI MJAMZITO AU

Image
Robyn Rihanna Fenty ‘Rihanna’. MWANAMUZIKI, Robyn Rihanna Fenty ‘Rihanna’ anadaiwa kuwa mjamzito kutokana na muonekano wake kifuani, usoni, matendo na mavazi.  Kwa mujibu wa mtandao mmoja umedai kuwa, Rihanna anadaiwa kushika ujauzito wa mpenzi wake Bilionea Hassan Jameel ambapo ameongezeka uzito wa pound 50 (kilo 23) tofauti na kawaida.  Julai Julai 25, mwaka huu Rihanna alionesha vazi lake jekundu lililoonekana la hadhi kubwa ambalo lilipendwa na wanamitindo alipokuwa kwenye maonesho huko London ndipo maneno ya kuwa mjamzito yalipoanza kuvuma huku watu wakidai kuwa maziwa yake na uso uliojaa ndiyo unaoonesha kuwa ni mjamzito.

NEYMAR AVUA JEZI NA KUONDOKA BARSELONA

Image
Mshambuliaji wa klabu ya Barcelona Neymar Dos Santos leo ametawala upya vichwa vya habari  baada ya kuvua jezi ya mazoezi ya Barcelona na kuondoka uwanjani.  Neymar alikuwa mazoezini na katika hali ya kawaida kulitokea kutokuelewana kati yake na mchezaji mpya wa klabu hiyo Nelson Semedo ndipo Neymar alipokasirika.  Neymar alionekana kutaka kumkabili Semedo lakini wakati anamfuata huku akionekana mwenye hasira ndipo Sergio Bosquet na Javier Mascherano walimzuia.  Baada ya Neymar kuzuiwa kuendeleza ugomvi alivua jezi maalumu ya mazoezi (bibs) akaitupa pembeni kisha akaupiga mpira kwa hasira na kuondoka zake.  Neymar amefanya tukio hilo katika kipindi hiki ambacho anahusishwa na uhamisho wa kwenda katika klabu ya PSG na huku ikitajwa kwamba hana furaha na Barcelona.  Tukio hili limezidi kuongeza tetesi kwamba Neymar anaweza kuondoka Barca lakini Barca kwa upande wao pia wamechoshwa  na tabia za Neymar haswa starehe zake.