Posts

Showing posts from June, 2017

Aliye kaa ardhini kwa siku 41 aibuka

MMOJA kati ya watu sita waliokaa siku 41 chini ya ardhi kufuatia kufunikwa na kifusi katika machimbo ya Nyangalata, wilayani Kahama mkoani Shinyanga, Chacha Wambura, anaomba msaada wa matibabu.  Wambura (51), alitembelewa na mwandishi wa habari hizi nyumbani kwake na kuomba msaada wa Sh. milioni 25 kwa ajili ya matibabu nchini India, baada ya matibabu yake kushindikana katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, jijini Dar es Salaam.  Akizungumza na gazeti hili mtoto wa Wambura, Marwa Chacha, alisema hali ya maisha nyumbani inazidi kuwa ngumu, licha ya kuishi maisha ya kimaskini na familia yao wako watoto 10 na wameishauza  ng’ombe 15 waliokuwa nao.  Kwa mujibu wa ripoti ya madaktari wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, alikotibiwa Wambura kwa miezi sita, ubongo wake upande wa kushoto umesinyaa na kusababisha mwili mzima kutetemeka, hali inayomfanya kuzungumza kwa taabu.  Wambura alifukiwa ndani ya machimbo ya Nyangalata, Oktoba 5 mwaka 2015, akiwa na wenzake Msafiri Gerald, Joseph Bulule na Amos

Rais MAGUFULI azidi kuungwa mkono na Madiwani CHADEMA Arusha

Image
Arusha.  Chadema mkoani Arusha, imeendelea kupata pigo baada ya diwani wa tano wa chama hicho kujiuzulu ndani ya mwezi mmoja naye kama wenzake, akisema anamuunga mkono Rais John Magufuli.  Akizungumza na waandishi wa habari jana, diwani huyo wa Muriet, Credo Kifukwe alitangaza kujiuzulu nafasi yake kutokana na kuridhishwa na utendaji wa Rais Magufuli.  Hata hivyo muda mfupi baada ya kikao hicho, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema alisema diwani huyo na wengine wanne waliojiuzulu katika Jimbo la Arumeru Mashariki linaloongozwa na Joshua Nassari wanashawishiwa kwa fedha na madaraka.  “Tuna taarifa kuna mkakati mkubwa wa kutumia fedha ambao unaendelea sio Arusha tu, ni kanda yote ya kaskazini, kununua viongozi waliochaguliwa lakini sisi kama Chadema hatuwezi kuwazuia wanaokubali kushawishiwa na kuondoka, kwani ni bora kubaki na viongozi wachache wenye moyo ya kuleta mabadiliko kuliko wengi ambao hawana dhamira ya kweli,” alisema.  Akizungumza katika kikao kifupi ofisini kwake, Kifukw

Mastaa waliohudhuria Harusi ya MESSI

Image
Mastaa waliohudhuria kwenye harusi ya Messi, Argentina   Friday, June 30, 2017     WACHEZAJI  wenzake wa sasa na wa zamani Lionel Messi katika timu ya Barcelona wamewasili Argentina kwa ajili ya harusi ya mwenzao huyo anayemuoa Antonella Roccuzzo kesho. Sergio Busquets, Jordi Alba, Carles Puyol, Cesc Fabregas, Xavi na Samuel Eto'o wote wameonekan katika picha iliyopostiwa kwenye ukurasa wa Instagram na mke wa Puyol, Vanessa Lorenzo. Messi amewakaribisha wenzake wote katika kikosi cha Barcelona kwenye sherehe hiyo mjini Rosario, ambako wageni wamekodiwa hoteli ya nyota tano. Mke wa Sergio Aguero, Karina ataimba wimbo wa kwanza katika sherehe hiyo. Messi pia ameagiza kipikwe chakula cha kiasili cha 'locro' na 'empanada' ambacho ni nyama rosti kabisa ya Kiargentina pamoja na 'maanjumati' mengine. Messi na mpenzi wake wa tangu utotoni hatimaye wataoana baada ya kukutana tangu wana umri wa miaka mitano mjini Rosar

Wavamia kanisa, wapiga walizi na kuiba

Image
KUNDI la watu wasiofahamika,  limevamia na kuvunja Kanisa la Mwanza City Center International Church Tanzania Reveland, lililopo Butimba mkoani Mwanza na kuanza kutembeza kichapo kwa walinzi na kuiba baadhi ya vifaa vya kanisa hilo,  Inaelezwa kwamba uongozi wa kanisa hilo ulikuwa na mgogoro na bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko kanda ya ziwa, huku kikundi cha wahalifu hao kikidaiwa kufanya uhalifu huo Juni 27 mwaka huu saa 11 alfajiri  .  Mama mzazi na Mchungaji wa kanisa hilo, Mama Moses Kulola ambaye ndiye mlezi wa Kanisa hilo, alisema alipigiwa simu na kuelezwa kuhusu kuvamiwa kanisa hilo huku akida  wavamizi hao walivunja ukuta na kuanza kuwapiga walinzi waliokuwa mlangoni.  Amesema kuwa baada ya kuanza kuwashambulia walinzi hao na kwamba walinzi hao walikimbia, na kuwapa nafasi ya kuingia ndani na kuiba viti, mabati na maiki zote, Spika na ngoma za kwaya zikibomolewa zote na wakatokomea kusikojulikana.  “Hii ni nyumba ya Mungu, najua heri ubomoe nyumba yangu mimi binafsi lak

Kisa cha aliyemuua nduguye kwa Mpini RUKWA

Image
Jeshi la Polisi mkoani Rukwa, linamshikilia mkazi wa kijiji cha Kilida Kona wilayani Sumbawanga, Japhet Kigula, kwa tuhuma za kumuua mdogo wake kwa kumpiga na mpini wa jembe kichwani wakati akimwadhibu.  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, George Kyando, aliwaambia waandishi wa habari jana ofisini kwake kuwa tukio hilo lilitokea Jumatatu wiki hii saa 12 jioni. Mtuhumiwa anadaiwa kumuua mdogo wake Makumbi Kigula.  Alisema chanzo cha mauaji hayo ni makumbi kutokwenda kwa kaka yake alipomwita ili wafanye mazungumzo ya kifamilia ambayo hayakuwekwa bayana baada ya mtukumiwa kurejea safarini kutoka Mwanza.  Baada ya kutokwenda wakati walikubaliana, alisema Makumbi alikwenda siku iliyofuata nyumbani kwa kaka yake hali iliyomfanya akasirike na kuchukua uamuzi huo.  Kutokana na hali hiyo, alisema Kigula akisaidiana na mmoja wa watumishi wake wa ndani walimkamata kijana huyo na kumfunga kamba mikononi na miguuni kisha  kaka mtu kuanza kumwadhibu kwa kutumia mpini wa jembe ambao alimpiga nao sehem

Ikulu Ya Rais nchini Brazil yanusulika kushambuliwa

Image
Dereva mmoja ajaribu kupitisha gari  lake kupitia lango kuu la makao ya ikulu ya rais nchini Brazil.  Hata hivyo dereva huyo aliweza kukamatwa baada ya vikosi vya usalama kupiga risasi gari hilo ingawaje dereva hakupata majeraha yoyote .  Rais Michel Temer hata hivyo hakukuwa katika ikulu hiyo.  Picha na video zilizotolewa zinaonyesha lango kuu la ikulu hiyo ya Alvorada likiwa na alama za risasi .  Rais Temer anakaa katika ikulu nyingine ya Jaburu maili moja kutoka ikulu ya Alvorada .

USHAURI WENU WADAU NA WASOMAJI WA BLOGG HII

Image
Hey wadau Ushauri wenu jee hii Rangi inapendeza au haipendezi ili uongozi uweze kuishughulikia,

Video :Navy Kenzo MORNING

Image

RATIBA Bundesliga yatolewa

Image
Ujerumani.  Mabingwa wa Bundesliga msimu wa 2016/17, Bayern Munich wamepagwa kuanza na Bayer Leverkusen mechi itakayochezwa Agosti 18.  Bayen Munich ilitwaa taji la ubingwa ikiwa mbele pointi 15 msimu ulioisha, huku ikipoteza mechi mbili pekee mechi 34 za mashindano yote ya ligi hiyo.  Mechi hiyo itapigwa kwenye dimba la Allianz Arena. Bayern Munich wataanza  kazi ya kutetea taji la ubingwa wakiwakaribisha timu hiyo iliyomaliza nafasi ya 12 kwenye msimamo wa Bundesliga msimu uliopita.  Shirikisho la Soka Ujerumani limetangaza ratiba hiyo ya msimu wa 2017/18 leo Alhamisi ambapo Borussia Dortmund watawafuata Wolfsburg ambao walinusulika kushuka daraja msimu uliopita.  RB Leipzig waliomaliza nafasi ya pili wataanza na Schalke ugenini huku wakitakiwa kujipanga vyema kwa ili kubakikwenye kiwango walichoonyesha msimu ulioisha

TAMBWE Aongeza mkataba wa miaka miwili YANGA

Image
 Mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi, Amissi Joselyn Tambwe (kulia) akisaini mkataba wa miaka miwili kuendelea kuichezea Yanga SC huku akishuhudiwa na viongozi wa klabu hiyo. Zoezi hilo limefantika makao makuu ya klabu, Jangwani, Dar es Salaam leo  Mhasibu Mkuu wa klabu, Baraka Deusdedit akimpekulia kurasa za kusaini Tambwe leo Jangwani

DAR ES SALAAM, Hatimae iPhone yatimiza miaka kumi

Image
Dar es Salaam.  Miaka 10 iliyopita siku kama ya leo Juni 29, 2007, Steve Jobs aliugeuza ulimwengu wa teknolojia ya mawasiliano ‘miguu juu’ baada ya kuzindua simu aina ya iPhone.  Leo hii simu hiyo inasherehekea miaka 10 tangu kuanzishwa kwake,     huku ikiwa ni  simu iliyouzwa kwa wingi kuliko zote katika dunia hii. Tangu kuanzishwa kwake zaidi ya simu za iPhone 1bilioni zimeuzwa katika masoko duniani.  Simu hizi zimebadilisha namna ya kuwasiliana, kufanya biashara, mazoezi, kusafiri, kufanya manunuzi na hata kutazama televisheni.  Kusherekea miaka 10, Gazeti la Mwananchi linakuletea mambo 10 ambayo huyafahamu kuhusiana na simu hii.   Ukitaka kupata undani wa mambo hayo, soma Jarida la Starehe katika gazeti letu Jumamosi hii.

MWALIMU afumwa akifanya mapenzi na mwanafunzi wake darasani

Image
Mkuu wa Wilaya ya Wanging'ombe, Mkoani Njombe, Ally Kasinge ameagiza kushikiliwa kwa Makamu Mkuu wa shule ya sekondari Wanike, iliyopo katika wilaya hiyo baada ya kukamatwa akifanya mapenzi na mwanafunzi wake darasani usiku.  Kasinge ametoa agizo hilo baada ya kuwepo taarifa ya kuwepo kwa watu wanaotaka kumsaidia mwalimu huyo kuvuruga ushahidi kwa kupanga na wanafunzi wenye ushahidi huo kuongea tofauti na tukio.  "Kuanzia wanafunzi walitimuliwa wahojiwe na polisi na wale wanafunzi wengine waliotajwa pia wahojiwe na polisi na mwalimu mwenyewe pia aendelee kushikiliwam huyo ambaye anatuhumiwa aendelee kushiliwa na polisi mpaka tupate majibu, kwa sababu akibaki nje ataendelea kutengeneza mazingira ya kutengeneza mtandao wa kutaka kumsaidia na kupotosha ushaidi" alisema Mkuu wa Wilaya Ally Kasinge  Mbali na hilo shule ya sekondari ya Wanging'ombe pamoja na Wanike zimepandishwa hadhi na sasa zitapokea wanafunzi wa kidato cha tano, walimu wa shule hizo wameweka wazi kuwa

MAWAKILI WAPYA 248 WAAPISHWA LEO

Image
 Mgeni Rasmi Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Hamis Juma (katikati) akifuatilia jambo wakati wa sherehe za 56 za kuwakubali na kuwasajiri, Mawakili wapya 248 mapema hii leo katika viwanja vya Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam.   Baadhi ya Mawakili wapya wakisubiri zoezi la kuapishwa mapema hii leo katika viwanja vya Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam.  Mgeni Rasmi Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Hamis Juma (wanne toka kushoto waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Majaji na Mawakili wapya mara baada ya kuwaapisha mapema hii leo katika viwanja vya Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam.  Kaimu Jaji Mkuu, Profesa Ibrahim Juma amewaasa mawakili kutokuwa mawakala wa kupeleka rushwa mahakamani badala yake wawe mawakala wa kutenda haki na kufuata maadili ya sheria.  Aidha, amewaasa mawakili hao wasome zaidi sheria za nje ya Tanzania ili pindi wanapotayarisha mikataba iwe mizuri kwa kuwa mikataba mingi inayoingiwa haitegemei sheria ya hapa nchini pekee.  Amey

Faiza Ally amchana makavu Hamisa Mobeto

Image
MSANII  wa sinema Bongo, Faiza Ally amemchokonoa Video Queen, Hamisa Mobeto baada ya kunasa kibendi na kusema kuwa, anamshangaa mwanadada huyo kwa kutochagua mtu stahiki wa kuzaa naye.  Akipiga stori na 3 Tamu, Faiza alisema kuwa, wasanii wengi hawajithamini miili yao na mfano mzuri ni mwanadada huyo ambaye anasikia ana ujauzito unaodaiwa ni wa msanii wa Bongo Fleva ambaye tayari ana familia yake na kuona alichofanya si sahihi.  “Unajua wasichana wengi hawajithamini wanafanya vitu bila kufikiria, kama huyo Hamisa nasikia ana ujauzito wa huyo msanii (jina kapuni) na kama ni kweli mimba ni ya huyo mtu, kakosea sana, napenda kuongea kitu kinachonigusa kwenye nafsi yangu akichukia atajijua,” alisema Faiza.  Msanii wa sinema Bongo, Faiza Ally

video:DIAMOND AAMUA KUUZA KARANGA

Image
Kama utakuwa na kumbukumbu vizuri April 21 Mwaka huu Msanii Huyo alizindua bidhaa yake kuuza Pafyum (Chibu Perfume). Leo Juni 29, Diamond Platnzumz akiwa Viwanja vya Karume Jijini Dar es salaam, Amezindua bidhaa yake mpya ya kuuza karanga alizozipa jina la "Diamond Karanga" kwa bei ya Shilingi mia tatu tu! TAZAMA FULL VIDEO HAPO CHINI...

VIDEO :Chris Brown celebrating

Image

VIDEO:Portugal vs Chile 5-2

Image

VIDEO :mauaji kibiti

Image

Jamali Malinzi hatoweza kushiriki uchaguzi TFF

Image
Rais wa TFF, Jamal Malinzi hataweza kutetea kiti chake cha urais.  Malinzi hataweza kwa kuwa kesi iliyomfikisha mahakamani leo itasikilizwa tena Jumatatu Julai 3 na Malinzi atakaa rumande hadi siku hiyo.  Usaili wa viongozi wanaogombea uongozi TFF unafanyika kuanzia leo hadi keshokutwa wakati huo Malinzi atakuwa mahabusu.  Malinzi amefikishwa leo mahakamani akiwa na katibu wake, Mwesigwa Celestine.  Baadhi ya mashitaka hayo ni kughushi waraka wa kamati ya utendaji ulioonyesha kuwa imeridhia kubadilishwa kwa Signatories (watu wanaosaini nyaraka za benki kutoa fedha). Shitaka hilo linawahusu Malinzi na Mwesigwa.  Malinzi amedaiwa kugushi risiti za kwamba anaidai TFF na ziko risiti 20 ambazo anatuhumiwa kuzifoji.  Shitaka jingine ni utakatishaji na hii wote watatu, Malinzi, Mwesigwa na Nsian wanatuhumiwa kutakatisha kiasi cha dola 375418