YANGA YASAJILI KIFAA HIKI HAPA.

Yanga Yamsajili Mshambuliaji  Yohana Mkomolwa Kutoka Serengeti Boys


SIKU moja baada ya kumsainisha mkataba wa miaka miwili beki wa kati raia wa Kongo, Fiston Kayembe, Yanga jana ilimnasa mshambuliaji wa timu ya Taifa ya Vijana 'Serengeti Boys' Yohana Mkomolwa.

Yanga inayodhaminiwa na Kampuni ya Kubashiri Matokeo Michezoni ya SportPesa, imemsainisha nyota huyo mkataba wa miaka miwili na ataanza kuitumikia timu hiyo pale ligi itakapoendelea baada ya kupisha michuano ya Kombe la Chalenji.

Mkomolwa ambaye alifanya vizuri na Serengeti Boys kwenye michuano ya Afrika iliyofanyika, Gabon mwaka huu,anakuwa mchezaji wa pili kusajiliwa na Yanga kwenye dirisha hili dogo.

Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh, akizungumza na gazeti hili jana, alithibitisha 'kinda' huyo kusajiliwa na Yanga.'Ni kweli Mkomolwa amejiunga na sisi..., na hii ni katika kuboresha kikosi chetu," alisema Saleh.

Katika hatua nyingine, Saleh, aliema kuwa kocha wa timu hiyo, George Lwandamina, ametoa mapumziko ya wiki moja kwa wachezji wake.

Alisema wachezaji wa timu hiyo wataendelea na mazoezi Jumatatu ijayo kwenye Uwanja wa Uhuru.

"Unajua baada ya ligi kusimama, kocha ameamua kuwapa wachezaji ambao hawamo kwenye vikosi vya timu za Taifa mapumziko ya wiki moja, tutaanza mazoezi Jumatatu ijayo,"alisema Saleh.

Yanga inawachezaji kwenye vikosi vya timu ya Taifa ya Tanzania Bara 'Kilimanjaro Stars' na ile ya zanzibar 'Zanzibar Heroes' ambazo zote zitashiriki michuano ya Chalenji inayoanza Desemba 5, mwaka huu nchini Kenya. 

Comments

Popular posts from this blog

Kubemenda Mtoto

Siwezi pitisha siku bila kutembea na malaya

HAYA NDIO MADHARA YA KUFANYA MAPENZI KWA NJIA YA MDOMO. (Oral sex).