WANAUME WAWE MBELE KUPIMA VVU


Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto dkt. Faustine Ndugulile akisisitiza jambo mbele ya Wadau na Watumishi wa Sekta ya Afya katika siku ya uzinduzi wa Mwongozo wa kutoa cheti kwa  maeneo ya kufanyia vipimo vya VVU  katika vituo vya kutolea huduma za Afya.
 Mkurugenzi wa Idara ya Uhakiki Ubora  toka Wizara ya afya Dkt. Mohamed Mohamed akimkaribisha mgeni rasmi mapema leo katika siku ya Uzinduzi wa Mwongozo wa kutoa cheti kwa  maeneo ya kufanyia vipimo vya VVU  katika vituo vya kutolea huduma za Afya. 
 Wadau wa masuala ya Afya wakifuatilia kwa ukaribu taarifa is juu ya Uzinduzi wa Mwongozo wa kutoa cheti kwa  maeneo ya kufanyia vipimo vya VVU  katika vituo vya kutolea huduma za Afya, tukio lililofanyika katika ofisi za NMRI jijini Da es salaam.
 Mwakilishi kutoka CDC Kevin De Cock akiwasilisha salamu kutoka CDC mbele ya Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto dkt. Faustine Ndugulile (wakwanza kushoto) katika uzinduzi wa Mwongozo wa kutoa cheti kwa maeneo ya kufanyia vipimo vya VVU  katika vituo vya kutolea huduma za Afya.
Mkurugenzi wa Idara ya Uhakiki Ubora  toka Wizara ya afya Dkt. Mohamed Mohamed (kushoto) akiteta jambo na Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto dkt. Faustine Ndugulile katika siku ya uzinduzi wa Mwongozo wa kutoa cheti kwa  maeneo ya kufanyia vipimo vya VVU  katika vituo vya kutolea huduma za Afya.
Picha ya pamoja ikiongozwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto dkt. Faustine Ndugulile katika siku ya uzinduzi wa Mwongozo wa kutoa cheti kwa  maeneo ya kufanyia vipimo vya VVU  katika vituo vya kutolea huduma za Afya, tukio lililofanyika katika ofisi za NMRI jijini Da es salaam.
**************************************
NA WAMJW-DAR ES SALAAM.
WANAUME  nchini wamesisitizwa kuwa kipaumbele katika kupima Maambukizi ya virus vya ukimwi (VVU) ili kusaidia juhudi za Serikali katika kupambana na vita dhidi ya maambukizo ya ukimwi.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati wa uzinduzi wa Kiunzi kazi wa Kutoa cheti kwa maeneo ya kufanyia vipimo vya VVU katika vituo vya kutolea huduma za afya.
“ Wanaume tumekuwa wagumu sana katika kupima maambukizi ya virusi vya ukimwi na tukikutwa tuna maambukizi tunatakiwa tuanze kutumia dawa za kufubaza  kuliko kuwasubiri wenza wetu kwenda kupima na sisi ndo tupate majibu yetu kupitia wao” alisema Dkt. Ndugulile.
Aidha Dkt. Ndugulile amesema kuwa katika kuhakikisha inapamabana na UKIMWI  wameweka taratibu ya kila mwananchi anayepima maambukizi ya Ukimwi na akagundulika kuwa na virusi hivyo anaanza dawa za kufubaisha mara moja.
Kwa mujibu wake Dkt. Ndugulile amesema kuwa mpaka kufikia 2020 Serikali inataka kufikia malengo ya kimkakati ya 90 90 90 ambayo 90 ya kwanza inamaanisha watu wapime VVU  kufikia asilimia 90, 90 ya pili inamaanisha wanaopima VVU kama wana maambukizi waanze kutumia dawa za kufubaza na 90 ya tatu inamaanisha wenye VVU wawe wamefubaza ugonjwa huo.
Aidha Dkt. Ndugulile ametoa rai kwa Watanzania wote kuchangia mfuko wa Udhamini wa kupamabana na Maambukizi ya Ukimwi kwa kupitia namba 0684909090 ili mradi kuweza kuongeza rasirimali fedha zitakazosaidia kwenye mapambano hayo.
Mbali na hayo Dkt. Ndugulile amesema kuwa katika kuelekea maadhimisho ya Siku ya ukimwi Duniani ambayo huadhimishwa Decemba 1 kila mwaka watu wote wajitokeze kupima VVU

Comments

Popular posts from this blog

Kubemenda Mtoto

Siwezi pitisha siku bila kutembea na malaya

HAYA NDIO MADHARA YA KUFANYA MAPENZI KWA NJIA YA MDOMO. (Oral sex).