OKWI. Sasa mambo safi tayari kuungana na wenzake mazoezini



Mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi anaweza kurejea nchini kati ya Jumamosi au Jumapili kuungana na wenzake.

Taarifa zinaeleza Okwi amepata nafuu kwa kiwango kizuri kabisa na anaweza kuanza mazoezi.

"Inawezekana akarejea wikindi hii, Jumamosi au Jumapili. Kama atakuwa fiti kabisa ataanza mazoezi Jumatatu," habari kutoka ndani ya Simba zimeeleza.

Lakini taarifa nyingine zinaeleza, pamoja na nafuu, Okwi anaweza kuchelewa kwa kuwa mkewe alikuwa amejifungua mtoto wa pili.

"Pamoja na kuwa majeruhi, kumbuka mkewe alijifungua. Hivyo anaweza kutaka kuhakikisha mambo yamekaa vizuri katika msitari kabla ya kuondoka," kiliongeza chanzo.

Comments

Popular posts from this blog

Kubemenda Mtoto

Siwezi pitisha siku bila kutembea na malaya

HAYA NDIO MADHARA YA KUFANYA MAPENZI KWA NJIA YA MDOMO. (Oral sex).