Posts

Showing posts from November, 2017

WANAUME WAWE MBELE KUPIMA VVU

Image
Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto dkt. Faustine Ndugulile akisisitiza jambo mbele ya Wadau na Watumishi wa Sekta ya Afya katika siku ya uzinduzi wa Mwongozo wa kutoa cheti kwa  maeneo ya kufanyia vipimo vya VVU  katika vituo vya kutolea huduma za Afya.   Mkurugenzi wa Idara ya Uhakiki Ubora  toka Wizara ya afya Dkt. Mohamed Mohamed   akimkaribisha mgeni rasmi mapema leo katika siku ya Uzinduzi wa Mwongozo wa kutoa cheti kwa    maeneo ya kufanyia vipimo vya VVU    katika vituo vya kutolea huduma za Afya.    Wadau wa masuala ya Afya wakifuatilia kwa ukaribu taarifa is juu ya Uzinduzi wa Mwongozo wa kutoa cheti kwa    maeneo ya kufanyia vipimo vya VVU    katika vituo vya kutolea huduma za Afya, tukio lililofanyika katika ofisi za NMRI jijini Da es salaam.   Mwakilishi kutoka CDC Kevin De Cock akiwasilisha salamu kutoka CDC mbele ya Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto dkt. Faustine Ndugulile (

Akifanya Gurdiola ni fresh tuu ila akifanya Mourinho ni noma

Image
Wazaramo wana misemo mingi lakini kuna msemo wanasema “sema wewe mirinda nkisema mimi pepsi nna gesi” wakimaanisha kwamba kuna mambo akifanya mtu huyu ni sawa lakini akifanya mtu mwingine ni kesi. Nimekumbuka msemo wa Wazaramo baada ya jana kumuona Mhispania Pep Gurdiola ambaye wiki chache tu zilizopita alitupiwa shutuma kwamba hana nidhamu na jana tena akaionesha dunia kwamba ana mihemko iliyopitiliza. Unakumbuka wakati Jose Mourinho akiwa katika eneo lake na akapiga kopo la maji baada ya kuona Pogba amepewa kadi kwa uonevu wakati wa mechi zidi ya West Ham? Refa hakufikiria mara mbili zaidi ya kumpa adhabu akaenda jukwaani. Achana na faini ambazo amekuwa hazikosi kila baada ya muda kadhaa lakini FA mara nyingi wamekuwa wakimmulika Mourinho na vitu vingi afanyavyo wamekuwa hawamuacho salama, kama sio onyo ni adhabu. Jana kumejitokeza tukio ambalo hii leo limekuwa mjadala mkubwa duniani baada ya Pep Gurdiola kupita eneo lake na kumfuata mchezaji Nethan Redmond na kuonekana wazi

CEKAFA CHALENGE CUP kuonyeshwa live Azam Tv

Image
KAMPUNI  ya Azam Media, imeingia mkataba na Baraza la Vyama vya Soka Afika Mashariki na Kati (CECAFA) kwa ajili ya kuonyesha mechi zote za michuano ya kombe la Chalenji, inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Desemba 3 hadi 16 mwaka huu nchini Kenya, yakishirikisha jumla ya timu tisa. Akizungumza na Wanahabari jana katika studio za Azam Tv, Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Kampuni hiyo, Tido Mhando, alisema kuwa, baada ya kuafanya vizuri katika Ligi Kuu Bara na mashindano mbalimba ya Ukanda wa Afrika Mashariki, zikiwemo nchi za Uganda, Rwanda na Kombe la Mapinduzi visiwani Zanzibar, Azam TV sasa imeamua kupiga hatua zaidi na kuingia katika michuano mikubwa zaidi Afrika. Alisema huo ni moja ya mipango ya Azam kwenye mikakati yao ya muda mrefu kuonyesha michuano mikubwa zaidi ya soka kwa ajili ya kujiandaa na michuano ya Mataifa ya Afrika kwa vijana (AFCON) wa umri chini ya miaka 17, itakayofanyika Tanzania mwaka 2019. “Kwa upande wetu maandalizi yanaendelea vizuri na timu nzima ya utayarisha

TANESCO yatolea ufafanuzi sababu ya Umeme kukata leo asubuhi Nchi nzima

Image
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Dkt. Tito Mwinuka, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, leo mchana kuhusu tatizo la umeme kukatika nchi nzima leo majira ya asubuhi, kutokana na mtambo wa kuzalisha umeme uliopo katika Gridi ya Taifa kupata hitilafu. Kushoto ni Kaimu Meneja Uhusiano wa Tanesco, Leila Mhaji. Picha na Muhidin Sufiani (MAFOTO)  Mkutano ukiendelea.. Kaimu Meneja Uhusiano wa Tanesco, Leila Mhaji, akizungumza kuwashukuru waandishi wa habari.

OKWI. Sasa mambo safi tayari kuungana na wenzake mazoezini

Image
Mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi anaweza kurejea nchini kati ya Jumamosi au Jumapili kuungana na wenzake. Taarifa zinaeleza Okwi amepata nafuu kwa kiwango kizuri kabisa na anaweza kuanza mazoezi. "Inawezekana akarejea wikindi hii, Jumamosi au Jumapili. Kama atakuwa fiti kabisa ataanza mazoezi Jumatatu," habari kutoka ndani ya Simba zimeeleza. Lakini taarifa nyingine zinaeleza, pamoja na nafuu, Okwi anaweza kuchelewa kwa kuwa mkewe alikuwa amejifungua mtoto wa pili. "Pamoja na kuwa majeruhi, kumbuka mkewe alijifungua. Hivyo anaweza kutaka kuhakikisha mambo yamekaa vizuri katika msitari kabla ya kuondoka," kiliongeza chanzo.

BREAKING NEWS! Rais Magufuli afanya uteuzi mpya

Image
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amteua Bi. Stella Tullo Chagi kuwa Msajili wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba wa Wilaya. Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Eng. John Kijazi ametangaza kuwa uteuzi huo Bi. Stella Tullo umeanza rasmi toka Novemba 25, 2017.

AVEVA NA MALINZI Kesi yao yazidi kupigwa kalenda

Image
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeziahirisha kesi za utakatishaji fedha inayowakabili Rais wa klabu ya Simba, Evans Aveva na ile inayomkabili aliyekuwa Rais (TFF), Jamal Malinzi hadi December 14,2017 kwa sababu upelelezi haujakamilika. Mwendesha Mashtaka wa Takukuru, Vitalis Peter amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri kuwa kesi ya Aveva na Malinzi zimeitishwa kwa ajili ya kutajwa na upelelezi wa kesi hizo bado haujakamilika. Baada ya kueleza hayo, Hakimu Mashauri ameahirisha kesi hizo hadi December 14/2017. Kwa pamoja washtakiwa hao wanadaiwa kuwa walikula njama ya kughushi fomu ya maombi ya kuhamisha fedha ya March 15,2016 wakionesha Klabu ya Simba inalipa mkopo wa  USD 300,000 kwa Evans Aveva wakati si kweli

Ahmed Albaity Aliyelala Kitandani Miaka 10 Asaidiwa na Makonda Kutibiwa kwa Milion 85 Nchini China

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amejitolea kumsaidia kijana Ahmed  Albaity  anayesumbuliwa na tatizo la uti wa mgongo lililompelekea kulala kitandani kwa takribani miaka 10. Kijana huyo anatakiwa kwenda kutibiwa nchini China kwa muda wa wiki tatu akiambatana na wasaidizi wawili ambapo gharama za matibabu zinazohitajika ni zaidi ya dola 40,000 za marekani ambapo sindano moja aliyoandikiwa inagharimu kiasi cha dolla 27,000. RC Makonda amesema atafanya jitihada zote kuhakikisha Ahmed anapatiwa Matibiwa ili aweze kupona na kutimiza ndoto zake akiwa na Afya Njema. Mapema leo RC Makonda ametembelewa ofisini kwake na Balozi mpya wa China Nchini Tanzania Bi. Wang Ke ambae amekuja kujitambulisha kwa Mkuu wa Mkoa ambapo katika mazungumzo RC Makonda amemgusia balozi huyo suala la matibabu ya AHMED ALBAITY ambapo Balozi WANG KE alieambatana pia na Daktari Bingwa wa China aliebaki Nchini kwaajili ya Shughuli ya Serikali ya China ambapo wamemtazama na kupitia Ripoti ambapo wameahidi

WQNAFUZI 106 WASITISHA MASOMO KWA KUPATA UJAUZITO

Image
Ukerewe. Wanafunzi 106 wa shule za msingi na sekondari wilayani hapa wamefukuzwa baada ya kubainika kuwa na ujauzito, wakati wa upimaji uliofanyika kati ya Januari na Aprili. Katibu tawala wilaya ya Ukerewe, Focus Majumbi alisema kati ya wanafunzi hao, wawili ni wa shule za msingi huku waliosalia wakiwa ni wa sekondari. “Sekondari ya Ilugwa iliyopo kisiwani, pekee ilikutwa na wanafunzi 11 wenye mimba,” alisema na kwamba, tayari wanaume 28 waliodaiwa kuwapa ujauzito wanafunzi hao wamefikishwa mahakamani. Ili kukabiliana na tatizo la mimba shuleni, wilaya  imeweka mikakati ikiwamo kupiga marufuku matamasha ya muziki nyakati za usiku maarufu Mazinduke. Naye mkuu wa Sekondari ya Ilugwa, Emmanuel Bomba alisema kati ya wanafunzi 11 waliobainika kuwa na ujauzito shuleni kwake, mmoja alipewa ujauzito na mjomba wake. Alisema kati ya wanafunzi 283 wa shule hiyo yenye mabweni mawili yanayochukua wanafunzi 96 kila moja, ni kumi pekee wazazi wao wamewalipia Sh480,000 za chakula na malazi. Shule h

SERIKARI YATOTEA UFAFANUZI JUU YA KONDOM MIL 500 ZITAKAZOSAMBAZWA KOTE NCHINI

Image
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imetoa ufafanuzi kuhusu taarifa ya serikali kusambaza kondom 500,000,000 katika kipindi cha miaka mitatu 2018 hadi 2020. Taarifa iliyotolewa na katibu wa wizara hiyo imeeleza kuwa Kumekuwa na taarifa mbalimbali, hamaki na kejeli zinazoenea katika mitandao ya kijamii kuhusiana na taarifa iliyotolewa tarehe 27 Novemba 2017, Mnazi Mmoja kwenye uzinduzi wa Mkakati wa Taifa wa Kondom kuhusu mpango huo wa Serikali. Tunapenda kuukumbusha umma wa Watanzania kwamba matumizi ya kondom ni moja wapo ya afua katika kuzuia maambukizi mapya. Hata hivyo utafiti wa viashiria vya Malaria na UKIMWI wa mwaka 2011/12 umebaini kuwa kuna matumizi duni ya kondom, kwani ni asilimia 27 tu ya watu wenye wenza zaidi ya mmoja waliokiri kutumia kondom mara ya mwisho walipofanya ngono. Hivyo Serikali itaendelea kununua na kusambaza kondom kwa lengo la kuzuia maambukizi ya VVU, magonjwa ya ngono na mimba zisizo tarajiwa ikiwa ni mojawapo ya afua hizo

Hizi ndizo sababu za Ngoma kusepa YANGA

Image
MSHAMBULIAJI WA TIMU YA YANGA, DONALD NGOMA HUKU mshambuliaji wa kimataifa wa mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga, Donald Ngoma, akiwa nje ya kikosi cha timu hiyo kutokana na kuelezwa kuwa ni majeruhi wa goti, imebainika kuwa sababu ni kutokana na kuidai klabu hiyo fedha za usajili. Akizungumza na Nipashe mmoja wa watu wa karibu na Ngoma (jina tunalihifadhi), alisema Ngoma ni mzima na kwamba yupo katika "mgomo baridi" wa kuitumikia Yanga ambayo inadhaminiwa na Kampuni ya Kubashiri Matokeo Michezoni ya SportPesa, akishinikiza kulipwa kwanza fedha zake za usajili kama walivyokubaliana. Chanzo hicho kilisema kuwa kutokana na Yanga kushindwa kutimiza makubaliano hayo licha ya Ngoma kusaini mkataba wa miaka miwili, mshambuliaji huyo amesema kuwa tayari mkataba waliosaini umevunjika rasmi. Aliongeza kuwa kutokulipwa kwa fedha hizo, kumemfanya mshambuliaji huyo kuchukua uamuzi wa kujiweka pembeni kwa sababu hapati majibu ya kueleweka kuhusiana na

Tabia za Mama Mkwe Ndio Tabia za Mkeo..Chukua hiyo Kubali Au Kataaa

Image
Kwa utafiti wangu mdogo niliofanya nimegundua kwamba tabia za mama mkwe ndio tabia za mkeo upende usipende.kwahiyo kama una mpango wa kuoa usiishie kumchunguza mchumba wa kike ambaye wakati wa uchumba anakuwa anaishi maisha ya kuigiza bali pia angaika kumchunguza mama mkwe. Kwanini mama mkwe? 1. Mama mkwe ndie aliyemlea mkeo mtarajiwa kwahiyo mchumba wako atakuwa ameiga na kufundishwa kuwa na tabia kama mama yake 2.Mara mwanamke anapoolewa Mshauri mkuu ni mama yake mzazi(napenda uamini hili) kwahiyo maisha yake kwenye ndoa yatategemea ushauri wa mamaye 3.ikitokea mfarakano kwenye ndoa na kama mwanamke ndio tatizo mama mkwe ndie mtu pekee anayeweza kumbadilisha mkeo katika njia sahihi

Uchambuzi wa Wimbo Mpya wa Diamond Platnumz Unaitwa Sikomi

Image
UCHAMBUZI WA WIMBO JINA LA WIMBO: SIKOMI MSANII : DIAMOND PLATNUMZ UTANGULIZI Diamond Platnumz ni msanii wa muziki wa kizazi kipya (bongofleva) kutoka Tanzania. Anaiwakilisha nchi yake na fasihi ya kiswahili nje na ndani ya nchi kwa ufanisi. Wimbo wake mpya wa Sikomi ni mojawapo ya nyimbo zake nyingi ambazo amepata kuziimba tangu alipoanza mziki wake. Ufuatao ni uchambuzi wa wimbo wa Sikomi. Angalizo uchambuzi huu utajikita zaidi kwenye vipengele vya maudhui na wala mhakiki hajagusa vipengele vya fani. DHAMIRA KUU Dhamira kuu katika wimbo wa Sikomi ni mapenzi. Msanii anaeleza historia yake ya kimahusiano toka alipotoka kimuziki mpaka hapa alipofika. Amegusia visa na mikasa aliyopitia katika mahusiano yake ya kimapenzi. Msanii amepitia katika mengi katika mapenzi lakini bado haachi kujihusisha na mapenzi huu ndiyo msingi wa jina la wimbo "Sikomi". Msanii anasema kila anapoumizwa na mwanamke mmoja anatafuta mwanamke mwingine wa kumfuta machozi. DHAMIRA NDOGO NDOGO US

Wanawake wengi 'Waliochelewa' Kuolewa Wameamua Kuokoka

Image
Idadi kubwa ya mabinti wa Kikristo ambao wamechelewa kuolewa, wengi wao sasa hivi ni mafull upako kuanzia post zao mitandaoni na hata maongezi yao. Ukiongea nao na kuomba appointment utasikia, 'siku hiyo tutakuwepo kanisani kwenye maombi'. Sijui hapo kuna siri gani nyuma ya pazia. Wameokoka kwa kuwa desperate au wameokoka kwa kuvutia wachumba au ni kweli wameamua kuyatoa maisha yao kwa Bwana?

HAJI MANARA ATANGAZA KUGOMBEA URAIS

Image
Msemaji wa Klabu ya Soka ya Simba Haji Manara, amesema anampango wa kugombea urais na anaamini atafanikiwa. Akipiga stori na Big Chawa kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Haji Manara amesema kazi zake anazofanya sasa zimemfanya aache hesima kubwa, kitu ambacho kinampa ujasiri wa kufikia uamuzi huo. “Unajua mi nakwenda kuwa rais wa nchi siku moja, mimi nakwambia Mungu akinipa uhai na majaliwa, nakwenda kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania”, amesema Haji Manara.

KIMENUKAA! Ndoa ya Dogo Janja na Uwoya yaanza kuyumba

Image
Kwa habari za kunyapia nyapia ni kwamba Irene Pancras Uwoya (Sheila Abdul) aanza kumchukia dogo janja kiasi cha kuyumbisha penzi lao na mbaya zaidi amekuwa akimnyima penzi dogo janja na mara nyingi hupenda kumkwepa kwepa janjaro na kiasi fulani anahisi kama janjaro ndo chanzo cha mumewe kipenzi Hamadi Kataut. Dogo janja mara kwa mara akitafutwa kujibu suala hili la kunyimwa penzi na uwoya amekuwa akibabaika sana na muda mwengine hupenda kujibu nje ya mada ili asiendelee kuulizwa

Diamond Atokisahau Alichofanyiwa na Wema na Penny

Image
Wakati msanii wa muziki wa Bongo Flava, Diamond Platnumz ameachia ngoma mbili kwa wakati moja ambazo ni Sikomi na Niache, ngoma ya kwanza imekuwa na nguvu na mapokeo makubwa kutokana na ujumbe uliyomo ndani yake. Katika ngoma hiyo ‘Sikomi’ Diamond amezungumzia maisha yake ya kimahusiano na wanawake maarufu kama Wema Sepetu, Penny na baby mama wake, Zari The Boss Lady. Wimbo huo wenye dakika 3:58 Diamond anaeleza baada ya kupambana kwa kipindi kirefu hadi kuja kutoka kimuziki aliamini pengine maisha yake ya kimahusiano yangekuwa vizuri kitu ambacho anakiri hakijamtokea tangu pale alipokutana na mrembo kutoka Bongo Movie. Licha ya kutomtaja mrembo huyo bila shaka anamzungumzia Wema Sepetu kwani ndiye mrembo pekee wa Bongo Movie aliyeanza kudate naye na couple yake kuwa na nguvu zaidi. Hata hivyo katika verse ya pili ya ngoma hiyo ndipo ameweka wazi kuwa anayemzungumzia ni Wema Sepetu kwa kueleza licha ya kumpenda sana lakini bado aliusumbua moyo wake. Moyo aliupatia mateso siwezi ku

JE Dada unapenda Kuwa Mrembo na Kaka Kuwa Lijari na Kumtosheleza Mpenzi Wako? 1

Image
BAADA YA UTAFITI TULIOFANYA MARKSON BEAUTY KWA KUSHIRIKIANA NA SHIRIKA LA AFYA DUNIANI (W.H.O) TUMEGUNDUA KUWA WANAUME WENGI DUNIANI HUSUMBULIWA NA MATATIZO KAMA👇👇 ☆Kukosa hamu ya tendo. ☆Kuwahi kufika kileleni na kushindwa kurudia tendo. ☆Maumbile madogo ya uume. ☆Kuchoka sana wakati wa tendo na uume kusinyaa nk. @markson_beauty_pr tumeandaa tiba bora kabisa kama ifuatavyo:- 1.HANDSOME UP OG_ Inaongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli (wiki 2) @250,000/= 2.SHARK POWER GELY_ Inaongeza uume inch 6 (wiki 4) @150,000/= 3VigRX CREAM_ Inaongeza uume inch 6.5 hadi 8 (wiki 2-3) @200,000/= 4.Vidonge maalum vya kuongeza nguvu na hamu ya tendo hata kwa wenye kisukari na BP @150,000/= 5.VIGA SPRAY OG_ Inaongeza uwezo ktk tendo na kuchelewesha kufika kileleni @150,000/= PIA KWA WANAWAKE WANAOPENDA KUWA NA MUONEKANO MZURI ZIPO ZA👇👇👇 ☆Kuongeza hips, makalio na mapaja @200,000/= ☆Kushepu mguu (CHUPA YA BIA) @150,000/= ☆Kuwa mweupe bila sugu @150,000/= ☆Kurefush

YANGA YASAJILI KIFAA HIKI HAPA.

Image
SIKU moja baada ya kumsainisha mkataba wa miaka miwili beki wa kati raia wa Kongo, Fiston Kayembe, Yanga jana ilimnasa mshambuliaji wa timu ya Taifa ya Vijana 'Serengeti Boys' Yohana Mkomolwa. Yanga inayodhaminiwa na Kampuni ya Kubashiri Matokeo Michezoni ya SportPesa, imemsainisha nyota huyo mkataba wa miaka miwili na ataanza kuitumikia timu hiyo pale ligi itakapoendelea baada ya kupisha michuano ya Kombe la Chalenji. Mkomolwa ambaye alifanya vizuri na Serengeti Boys kwenye michuano ya Afrika iliyofanyika, Gabon mwaka huu,anakuwa mchezaji wa pili kusajiliwa na Yanga kwenye dirisha hili dogo. Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh, akizungumza na gazeti hili jana, alithibitisha 'kinda' huyo kusajiliwa na Yanga.'Ni kweli Mkomolwa amejiunga na sisi..., na hii ni katika kuboresha kikosi chetu," alisema Saleh. Katika hatua nyingine, Saleh, aliema kuwa kocha wa timu hiyo, George Lwandamina, ametoa mapumziko ya wiki moja kwa wachezji wake. Alisema wachezaji wa timu hiyo

MAGAZETINI LEO TAREHE 27/11/2017

Image