Wizi wa Miundombinu ya Umeme, Wananchi wa iomba Tanesco kukamilisha Fidia


Wananchi wa Kijiji cha Misigiri, Tarafa ya Ndago,Wilayani Iramba,Mkoani Singida wameliomba shirika la ugavi umeme Tanzania (TANESCO) kukamilisha malipo ya fidia kwa wananchi 17 wa Kijiji hicho ambao maeneo yao yamepitiwa na njia kuu ya umeme wa KV 400 kutoka Mkoani Iringa hadi Shinyanga ili waweze kuondoa chuki kati yao na shirika hilo na hivyo kuwa walinzi wakubwa wa miundombinu iliyowekwa kwenye njia hiyo.

Wananchi hao, Kanasi Peter, Boniface Nzenga, Mwita Wilson Makanga na Helena Yuda wamesema vitendo vya uharibifu na wizi wa miundombinu ya shirika hilo vinasababishwa na shirika hilo kutowalipa wananchi hao madai yao ya fidia kutokana na njia kubwa ya umeme kupita kwenye maeneo waliyokuwa wakilima na hivyo kuwafanya waendelee kufanya shughuli za uzalishajimali zilizokuwa zikiwaingizia kipato.

Malalamiko hayo yametolewa na wananchi wa Kijiji cha Misigiri,Tarafa ya Ndago wakati uongozi wa shirika la TANESCO ulipokwenda kutoa elimu kwa wananchi hao juu ya kushirikiana na shirika hilo kulinda wizi pamoja na uharibifu wa miundombinu ya shirika hilo.

Comments

Popular posts from this blog

Kubemenda Mtoto

Siwezi pitisha siku bila kutembea na malaya

HAYA NDIO MADHARA YA KUFANYA MAPENZI KWA NJIA YA MDOMO. (Oral sex).