Waziri Mwakyembe Achimba Mkwara ‘Mazoea’ Taifa Stars


Waziri mwenye dhamana ya michezo Tanzania Dr. Harrison Mwakyembe amesema suala la uwakilishi kwenye timu ya Taifa kwa mazoea inabidi liangaliwe kwa makini kwa sababu kuna wachezaji wamekuwa na uhakika wa kuitwa kwenye timu hata kama hawajitumi wakiwa kwenye timu hiyo.

Waziri Mwakyembe amesema hata yeye ameumizwa na matokeo yaKilimanjaro Stars kwenye Challenge Cup kufuatia mfululizo wa matokeo mabovu ambapo timu hiyo haikushinda hata mechi moja kati ya nne ilizocheza hatua ya makundi huku ikitupwa nje ya mashindano ikiwa na pointi moja iliyoipata baada ya suluhu dhidi ya Libya kwenye mechi ya kwanza.

“Sasa uwakilishi kwenye Taifa Stars kwa mazoea hili suala lazima tuliangalie kwa makini sana. Sio mchezaji anakuwa anauhakika wa kuitwa kwenye timu, tunataka tuone kwa kujituma”-Mwakyembe.

Mwakyembe pia amesema kutokana na wachezaji wa Zanzibar Heroes wanavyojituma kwenye michuano ya Challenge Cup 2017, anaamini watarudi na kombe hilo.

“Kwa mchezo wanaouonesha vijana wa Zanzibar Heroes nina uhakika hili kombe tunalipata, litakuja Tanzania. Wanacheza kwa kujituma, sio mtu anacheza kwa kujituma nusu kwa sababu atajituma zaidi akiwa kwenye klabu, nafiri nimejifunza vizuri sana kama Waziri katika sekta hii.” 

Comments

Popular posts from this blog

Kubemenda Mtoto

Siwezi pitisha siku bila kutembea na malaya

HAYA NDIO MADHARA YA KUFANYA MAPENZI KWA NJIA YA MDOMO. (Oral sex).