MKE WA KAFULILA AFUNGUKA TENA

November 30, 2017 Mbunge wa Viti Maalum kupitia CHADEMA Jesca Kishoa ambaye pia ni Mke wa Mbunge wa zamani Kigoma Kusini David Kafulila amekuwepo kwenye headlines kwa zaidi ya wiki moja baada ya Kafulila kuhamia CCM na kumuacha CHADEMA.

Kupitia page yake ya Instagram Jesca ameandika yafuatayo…

UCHAGUZI HUU WA UDIWANI UTOSHE 
KUTOA PICHA HALISI YA TAIFA HILI KWA SASA.

Mungu katunyima binadamu kujua siri nyingi za dunia hii ili turudi kwake na kumtambua yeye peke yake kama Mfalme wa ulimwengu.

Ametunyima kuchagua wazazi wa kutuzaa (maana uwenda wengine wangetaka kuzaliwa na watu wa aina ya Trump au Dangote,) ametunyima kuchagua wapi pa kuzaliwa (maana wengine uwenda wangetamani kuzaliwa ulaya na sio Tanzania)

Ametunyima kuchagua malezi ya kulelewa na ndio maana kwa mazingira yoyote watoto wamekuwa wakiishi kutegemeana na mazingira ya wazazi.

Lakini Mungu ametupa nguvu moja kubwa ambayo ikitumika vema huleta matunda mema na majibu ya mambo yote niliotaja juu, Mwenyezi Mungu katika maandiko matakatifu amezitambua Serikali za wanadamu na kupitia hizo endapo kutapatikana viongozi sahihi waliochaguliwa na wengi, ambao kwa uwingi huo ni alama au tafsiri ya chaguo la Mungu, hakika nchi itaneemeka na itatulia.

Ikiwa kinyume chake kwamaana ya alieshinda kuanzia mbinguni sie aliepewa ushindi duniani hakika mambo hugeuka kuwa laana na mateso kwa viumbe wa Mungu, Anguko la Madiwani au Wabunge wanaoshinda chaguzi sio la kwao peke yao na vyama vyao ni anguko la watu wa Mungu waliopaza sauti zao kwa unyenyekevu kupitia sanduku la kura.

WOTE KWA PAMOJA TUKEMEE VIKALI UPINDISHAJI WA MATOKEO BILA KUJALI WEWE NI NANI NA UNA UHUSIANO GANI NA SIASA ZA NCHI ILI KULIOKOA TAIFA HILI.

Roho mtakatifu ana uwezo mkubwa na nafasi kubwa ya kunyoosha mambo sawasawa, ungana na mimi katika maombi maalum juu ya taifa hili usiku huu kabla hujalala popote ulipo – hayo ndio aliyoyaandika Jesca.

Comments

Popular posts from this blog

Kubemenda Mtoto

Siwezi pitisha siku bila kutembea na malaya

HAYA NDIO MADHARA YA KUFANYA MAPENZI KWA NJIA YA MDOMO. (Oral sex).