YANGA YAMKINGIA KIFUA BEKI WAKE MKONGOMAN. Yatoa sababu kwanini hayupo mpaka sasa.



Klabu ya soka ya Yanga imetoa sababu kwanini mlinzi wake mpya wa kimataifa Fiston 'Festo' Kayembe Kanku ameshindwa kujiunga na timu tangu asajiliwe Disemba 2017.

Akiongea leo Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Hussein Nyika amesema mchezaji huyo raia wa DR Congo hajajiunga na timu kwasababu anashughulikia matatizo ya kifamilia.

“Kanku ana matatizo makubwa ya kifamilia ndiyo maana tumempa ruhusa ya kwenda kuyashughulikia, akimaliza atakuja kuanza kazi, na atacheza tu ligi bado ina mechi nyingi sana,”amesema Nyika.

Kwa upande mwingine Nyika ameongelea suala la uhamisho wa kimataifa (ITC), amabapo ameeleza kuwa ulikuwa unasumbua ila kwasasa wapo kwenye hatua za mwisho kuupata japo kuwa tayari mchezaji huyo ni mali ya Yanga.

Mabingwa hao watetezi wa ligi kuu soka Tanzania Bara wanashika nafasi ya 5 kwenye msimamo wakiwa na alama 22 kwenye mechi 13 walizocheza huku kesho wakishuka dimbani kucheza na Ruvu Shooting.

Comments

Popular posts from this blog

Kubemenda Mtoto

Siwezi pitisha siku bila kutembea na malaya

HAYA NDIO MADHARA YA KUFANYA MAPENZI KWA NJIA YA MDOMO. (Oral sex).