Posts

Showing posts from March, 2018

PANYA ROAD WAILUKU WAVAMIA NA KUPORA MALI.

Image
Kwa mara nyingine tena taharuki, hofu na wasiwasi mkubwa viliwakumba wakazi wa Tabata wilayani Ilala jijini Dar es Salaam kwa takribani saa tatu baada ya kundi maarufu la uporaji la Panya Road kuvamia mitaa mbalimbali na kupora mali. Kundi hilo lililokuwa na vijana zaidi ya 30 waliokuwa wameshika nondo, visu, mapanga na bisibisi jana usiku Machi 29,2018 lilisababisha wakazi wa Tabata Kisiwani, Kimanga hadi Kinyerezi kujifungia majumbani mwao na baadhi kujifungia ndani kutokana na jinsi kundi hilo lilivyokuwa likivamia biashara na nyumba kupora. Mmoja wa mashuhuda wa eneo la Tabata Kisiwani, Isaya Subi amesema tukio hilo lilianza saa mbili usiku ambapo kundi hilo lilivamia katika eneo hilo, kupora mali mbalimbali kwenye maduka pamoja na kuwapora wapita njia. “Vijana hawa si mchezo walikuwa kama 30 hivi kila mmoja alibeba nondo, bisibisi, wembe na spoku wakikukuta njiani wanakupiga huku wakikusachi na kuchukua kila kitu ulichokuwa nacho wengine walivamia maduka na kuchukua bidhaa

MSUVA AFUNGUKA KUTAKA KUUZWA KWA BIL. 1.3

Image
SIMON Msuva ni kiungo mshambuliji wa timu ya Diffaa Al Jadi­da ya nchini Morocco ambaye ametua katika klabu hiyo mwanzoni mwa msimu huu akitokea Yanga. Msuva ni miongoni mwa wachezaji wachache wa Kitanzania wanaowakilisha nchi nje ya nchi wakicheza soka la kulipwa ambapo ameonyesha uwezo wa hali ya juu katika katika klabu yake hiyo kutokana na ubora wake katika kuzoea mazin­gira mapema na kuwa mfungaji mzuri. Alijiunga na Al Jadida, Julai 29, mwaka jana kwa dau la dola 150,000 ambalo ni zaidi Sh milioni 337 akitokea Yanga la­kini kwa sasa Waarabu wamemthamin­isha kwa euro 475,000, sawa na zaidi ya Sh bilioni 1.3. Moja ya mikakati yake ni kuona anafanikiwa kusonga mbele zaidi ili aweze kumfikia Mtanzania mwen­zake, Mbwana Samatta anayekipiga katika Klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji. Championi Ijumaa imefanya mazun­gumzo na kiungo huyo ambaye ameelezea mikakati yake pamoja na kupanda kwa tha­mani yake kwa sasa. Mazungumzo hayo ilikuwa ni baada ya mchezo wa Taifa Stars dhidi ya DR Congo kwe

KAGAME CHALLENGE CUP NDANI YA TANZANIA.

Image
Michuano ya klabu bingwa ya Afrika Mashariki na Kati inayosimamiwa na Baraza la vyama vya soka ukanda huo (CECAFA) maarufu kama Kagame Cup yanatarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam mwezi Juni mwaka huu. Michuano hiyo inarejea baada ya kupita miaka mitatu kufuatia kukosena kwa wadhamini huku bingwa mtetezi akiwa Azam FC. CECAFA imepokea kiasi cha dola Milioni moja kutoka Shirikisho la soka duniani (FIFA) ili kufanikisha mashindano mbalimbali yakiwemo ya vijana chini ya umri wa 17 yatakayofanyika nchini Burundi, pamoja yale ya Wanawake na Wanaume kwa nchi wanachama. Taarifa za ndani kutoka katika uongozi wa CECAFA zinasema kuwa michuano hiyo itafanyika kati ya Juni 30 hadi Julai 14 jijini Dar badala ya Djibouti kama ilivyotangazwa awali. Taarifa zimezidi kusema kuwa michuano hiyo ilipangwa kufanyika nchini Djibouti lakini Azam TV ambao wameingia mkataba kurusha matangazo hayo moja kwa moja wameshauri kubadilishwa kutokana na sababu za kiusalama. Simba ndio inaongoza kwa ku

BAO LA SAMATTA LALETA UTATA CONGO.

Image
Mashabiki wa DR Congo wameamsha sekeseke kwa shirikisho la soka nchini humo wakidai halikuwa na maandalizi mazuri na timu yao. Hii inatokana na kero ya kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Tanzania na hasa lile bao na nahodha, Mbwana Samatta. Wengi wa mashabiki waliotoa maoni yao katika kipindi cha Okapi Radio wamelaani kitendo hicho, Mtanzania Rashid Said anayeishi nchini Congo amesema wamekuwa wakilalamika sana na hasa bao la Samatta. “Unajua huku hawaelewani sana na hasa maeneo, mfano hapa Lubumbashi na Kinshasa ni mbali sana na watu wana maisha tofauti utafikiri ni nchi mbili tofauti. “Lakini linapofikia suala la mpira, wanaungana na wanazungumza lugha moja. Hawakupenda kufungwa na Tanzania lakini kufungwa na Samatta kumewaudhi zaidi. “Wanalalamika sana na katika maoni yao wanataka hata viongozi wa shirikisho lao waachie ngazi,” alisema. Samatta alifunga bao la kwanza katika mechi hiyo ya kirafiki kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, huku Shiza Kichuya akimalizia kazi kwa kufu

HABARI MPYA KUTOKA NDANI YA WANAJANGWANI LEO HII.

Image
Habari mpya kutoka ndani ya Yanga ni juu ya mkutano mkuu kwa wanachama wote. L see Bofya hapa kupata taarifa zaidi kuhusu mkutanohuo USISAHAU KUSUBSCRIBE. 

BAADA YA MECHI. WACHEZAJI WA YANGA WALIOKUWA KWENYE KIKOSI CHA TAIFA STARS WATIMKIA MOROGORO WA WENZAO KAMBINI

Image
Wachezaji wa Yanga waliokuwa kambini na timu ya taifa, Taifa Stars, leo wanatarajia kusafiri kuelekea mkoani Morogoro kujiunga na kikosi chao kinachojiandaa na mchezo wa Kombe la FA dhidi ya Singida United. Yanga imeweka kambi Morogoro kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Singida United utakaopigwa Aprili Mosi 2018 kwenye Uwanja wa Namfua, mjini Singida. Ibrahim Ajib, Hassan Kessy, Kelvin Yondan na Gadiel Michael wataondoka mchana wa leo kwenda Morogoro kuungana na wachezaji wenzao ambao wameweka kambi maalum mjini humo. Golipika Ramadhan Kabwili, hatoweza kusafiri kutokana na majukumu mengine ya kuitumikia timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 20, Ngorongoro Heroes, inayojiandaa na mchezo wa kufuzu kuelekea AFCON U20. Ngorongoro inajiandaa kucheza mchezo wa kuwania kufuzu kwa fainali za AFCON U20 dhidi ya DR Congo Machi 31 2018 utakaopigwa katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam

Vituo vya Redio 23 Vyafungiwa kwa 'Kutangaza Uganga wa Kienyeji

Image
Tume ya mawasiliano nchini Uganda, UCC, imefungia zaidi ya vituo 20 vya redio vya FM. Vituo hivyo vinashutumiwa kutangaza 'uganga wa kienyeji na kuwatapeli wananchi.' HATUJAMALIZA BY@lantanatz live today on 5select EATV Hatua hii inafuata onyo la tangu zamani viache kuwaweka hewani waganga wa kienyeji. Tangazo hilo la kufungiwa vituo vya redio 23 limetolewa jana jioni na mwenyekiti wa Tume ya Mawasiliano Godfrey Mutabazi. Bwana Mutabazi ameshutumu redio hizo kutumiwa na waganga wa kienyeji kuwatapeli wananchi na kuvunja sheria ya uchawi ya kifungu cha pili. Redio hizo zimekuwa zikiwapa vipindi waganga hao wa kienyeji kutangaza uganga wao, huku wakiwaambia wananchi kutuma fedha kupitia njia ya simu za mikononi. Msemaji wa tume ya mawasiliano Pamela Ankunda ameielezea BBC kuwa, "Kwa kuwaweka hewani matapeli wanaojiita waganga wa kinyeji, wakitumia mbinu mbali mbali wakiwa hewani ili kuwatepeli wananchi." "Kwa mfano kwa kuwalaghia wananchI kwamba ukit

HAYA HAPA MANENO ALIYOSEMA MANARA BAADA YA KAPOMBE KUTUPIA MPIRA GOLINI KWAKE LA KUJIFUNGA.

Image
Kama kawaida yetu ni kukupenyezea yaliyojili kote Dunia Leo nipo na Hili hapa aliloliandika Msemaji wa Simba SC. HAJI S MANARA. Baada ya kapombe kujifunga goli wakati wa mechi ya kirafiki dhidi ya Algeria. Maneno ya mtaani yamemfanya msemajihuyo wenda kuisaidia vibaya na kuamua kukumbushia tukio kama hilo alilowahi kulifanya beki wa Watani wao YANGA. HAJI alionekana kuandika kama ifuatavyo USISAHAU KUFUATIA KIPINDI CHA 5select siku ya JUMATANO kumsikiliza na kumwona msanii mpya anayetamba na kibao chake kinacho itwa HATUJAMALIZA.

MBWANA SAMATTA AFUNGUKA HAYA KUHUSU MECHI ZA KIRAFIKI.

Image
Nahodha wa Taifa Stars ambaye anayekipiga kwenye klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji, Mbwana Samatta amesema ipo haja ya kuwepo mechi za kirafiki nchini kwa madai kitendo hicho kitapelekea kuwajenga vizuri wachezaji wa ndani pamoja na kuwapa uzoefu mkubwa. Samatta ametoa kauli hiyo muda mchache ilipomalizika mechi yao dhidi ya DR Congo (The Leopards) kwenye mchezo wa kirafiki wa kalenda ya FIFA kwa mwezi Machi uliomalizika ikiwa Stars wamepata ushindi wa mabao 2-0 mtanange uliyochezwa kwenye uwanja wa taifa Jijini Dar es Salaam. "Mechi hizi za kirafiki nafikiri Tanzania wanazihitaji kwa sana japokuwa ni 'game' ngumu lakini mwisho wa siku unapopata matokeo mazuri yanasaidia kukusogeza kwa kiasi fulani katika viwango vya FIFA, pia hata usipopata matokeo mazuri yanaweza kukusaidia kukujenga katika kujiamini na uzoefu zaidi", amesema Samatta. Pamoja na hayo, Mbwana Samatta ameendelea kwa kusema "ni michezo ambayo tunaihitaji katika kuwajenga wachezaji wetu wa tanzania ha

MA GAZETA YA LEO JUMATANO TAR 28/03/2017.Ngoma na Kamusoko wapishana Yanga.

Image

WACHEZAJI WETU WANA HASIRA SANA SINGIDA UNITED KUWENI MAKINI.

Image
Baada ya kukaa nje kwa karibu nusu msimu kutokana na majeruhi, wachezaji Donald Ngoma, Amissi Tambwe na Thabani Kamusoko wamerejea kwenye kikosi cha Yanga kikamilifu. Alianza kurejea Tambwe akaumia, akafuata Kamusoko na sasa Tambwe na Ngoma wamerejea kikamilifu tayari kuisaidia Yanga kutwaa taji la ligi kuu ya Vodacom kwa msimu wa nne, kutwaa kombe la FA pamoja na kutinga makundi kombe la Shirikisho. Wachezaji hao tayari wameanza mazoezi na kikosi cha Yanga huku pia wakifanya mazoezi ya ziada ya Gym ili kuhakikisha wanakuwa 'fiti' kuhimili mikiki mikiki ya michuano yote. Yanga iko kambini mkoani Morogoro kujiandaa na mchezo wa robo fainali kombe la FA (ASFC) dhidi ya Singida United unaotarajiwa kupigwa siku ya pasaka, April 01. Kurejea kwa watatu hao ni habari njema sana kwa kikosi cha Yanga kuelekea mchezo huo kwani sasa Singida United itakumbana na Yanga iliyokamilika kwelikweli. Yanga na Singida United tayari zimekutana mara tatu msimu huu. Zilikutana mara ya kwanza

SINGIDA UNITED YAJIBU MAPIGO YA YANGA.

Image
Klabu ya soka ya Singida United imejibu mapigo ya maandalizi ya mchezo wake wa robo fainali ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Yanga kwa kuweka kambi mbali na dimba lao la Namfua mkoani Singida. Taarifa ya klabu hiyo imeeleza kuwa kikosi hicho kimeondoka katikati ya mji wa Singida na kuelekea pembezoni mwa Mkoa huo kwaajili ya kujiandaa kuelekea mchezo huo utakaopigwa April 1, 2018. Wakati Singida wakifanya hivyo mabingwa wa soka nchini Yanga, nao wameondoka jijini Dar es salaam jana kuelekea mkoani Morogoro ambako itaweka kambi kwaajili ya maandalizi ya mchezo huo. Kambi za Singida United na Yanga zote zinawakosa wachezaji wao ambao wapo kwenye kikosi cha timu ya taifa ambayo leo inashuka dimbani kucheza na DR Congo kwenye mchezo wa kirafiki wa kalenda ya FIFA. Singida United inamkosa nahodha wake Mudathir Yahya wakati Yanga inawakosa Ibrahim Ajib, Kelvin Yondani, Hassan Kessy, Gadiel Michael na Ramadhani Kabwili. Wachezaji hao watajiunga na timu zao baada ya mchezo wa leo

HABARI NJEMA KWA WANAJANGWANI. Yanga ya Pata mwaliko mpya wa kushiriki mashindano nchini KENYA.

Image
Hii ni inaweza kuwa Habari njema kwa kwa wanajangwani, kupata Fursa ya kushiriki michuano mbalimbali. Yanga Inayoshiriki michuano mitatu mpaka sasa, Habari kutoka ndani ya klabu hiyo ni mwaliko walioupokea kutoka nchini Kenya kwenda kushiriki michuano ya SportPesa, ambayo imeandaliwa na wadhamini hao. SportPesa ni wadhamini wa Yanga pia katika ligi Kuu VPL na mpaka sasa Yanga itafikisha jumla ya michuano minne(4). Ikiwemo VPL, FA cup, Shirikisho barani Afrika, na SportPesa.

HATUA ZA KUFUATA WAKATI WA KUFANYA MAPENZI.

Image
WAPENZI na wanandoa wengi hivi leo wanapoingia kitandani tayari kwa kuianza safari ya kupeana haki zao za msingi hushindwa kufurahia tendo na hasa hali hii hujitokezwa kwa wanawake kwani mwanaume huwa na haraka iliyopitiliza!  Mwanaume atamkumbatia na kumbusu mwanamke kwa muda mfupi na kabla hata hamasa ya mapenzi ya mwanamke ahaijashika hatama, atamwingilia na ndani ya dakika sekunde ama dakika zisizozidi 3, mwanamme hufika mshindo. Katika hali ya kusikitisha baada ya mwanaume kujitosheleza hujongea pembeni bila kujali mwenza wake hajaf ika mwisho wa safari hali inayosababisha mwanamke kupoteza hamu ya tendo endapo endapo tabia hiyo ya mwanaume itaendelea. Kunahatua nne muhimu ambazo wapendanao wakizishika na kuzitekeleza ipasavyo basi watafanikiwa kujitosheleza kila wanapokutana na kwa hakika watakuwa miongoni mwa watu wachache wanaofurahia faragha kila wakutanapo! Hatua ya kwanza ni kusameheana: Wanandoa wengi hushindwa kupata raha ya mlo wa usiku kutokana na ku

JE HISTORIA ITAJIRUDIA TENA TAREHE 29 APRIL 2018,Pale taifa.

Image
Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara kupitia Mtendaji Mkuu, Boniface Wambura leo imetangaza rasmi tarehe ambayo Watani wa Jadi (Simba SC na Yanga SC)watacheza. Timu hizo sasa zitacheza tarehe 29 Aprili 2018 katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mechi ambayo Simba atakuwa mwenyeji wa pambano hilo. Awali Bodi ya Ligi ilikuwa haijaweka tarehe hiyo wazi kutokana na mambo mbalimbali kuingiliana na kufanya ratiba ya mchezo huo kutopangwa kwa wakati. Timu hizi zenye wafuasi wengi nchini, zilikutana Oktoba 28 2017 kwenye mzunguko wa kwanza wa ligi na kwenda sare ya bao 1-1, huku wafungaji wa mabao hayo wakiwa ni Shiza Kichuya upande wa Simba na Obrey Chirwa kwa Yanga