Posts

Showing posts from February, 2018

MSIMAMO VPL BAADA YA MECHI YA LEO.simba Vs Mbao Fc

Image

HIZI NDIZO SALAMU ZA MBAO KWA SIMBA LEO.

Image
Kikosi cha Mbao kimeamua kupeleka salamu kwa wapinzani wao Simba kuelekea mchezo wao wa leo Jumatatu utakaopigwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kwa kusema kuwa wamekuja jijini Dar es Salaam kupata ushindi na si vinginevyo. Mwenyekiti wa timu hiyo, Solly Zephania Njashi, alisema kuwa maandalizi yao ya mchezo wa leo yapo vizuri na wamejiandaa vya kutosha na wamekuja kwa ajili ya kupata ushindi. “Sisi tumejiandaa vizuri kwa ajili ya mchezo wetu wa kesho (leo) na mashabiki wafike kwa wingi kwani tuna uhakika tutaibuka na ushindi, tumejipanga kuhusu hilo. “Sisi tumekuja kupata ushindi, siyo kupoteza, sema tatizo huwezi jua naye mpinzani wako amejipanga vipi kwenye mchezo huo, lakini sisi tupo vizuri na kikosi hakina majeruhi, bali kuna mmoja tu ambaye tulimpandisha kutoka kwenye academia, ila mwalimu atatoa ripoti kama atacheza au la,” alisema Njashi.

DANTE AJITOA YANGA DK 180

Image
By KHATIMU NAHEKA BEKI wa kati wa Yanga, Andrew Vincent ‘Dante’ yuko jijini Dar es Salaam akiendelea na matibabu, lakini ametoa picha ya lini atarudi uwanjani kuendelea na majukumu yake, huku akikosa mechi mbili ukiondoa ya kesho ya kimataifa nchini Shelisheli. Dante aliliambia Mwanaspoti bado anaendelea na tiba katika moja ya hospitali inayosimamiwa na raia wa China akiuguza majeraha yake ya nyama za paja. Alisema kutokana na matibabu anayoendelea nayo atazikosa mechi mbili zijazo, dhidi ya Majimaji utakaopigwa mjini Songea ukiwa ni mchezo wa 16 Bora wa Kombe la FA na ule wa Ligi Kuu dhidi ya Ndanda mjini Mtwara. Beki huyo mbishi alisema kutokana kupungua kwa maumivu kadri muda unavyosogea, huenda akarudi kazini katika mchezo wa ugenini dhidi ya Mtibwa Sugar ya Morogoro. “Kwa sasa naendelea vizuri kidogo japo bado nipo kwenye matibabu. Naona yananisaidia, hata hivyo, niliongea na daktari wangu na ameniambia sitaweza kucheza mechi mbili zijazo,” alisema D

MCHEZAJI HUYU WA YANGA AUGUA GHAFLA, SASA NI HATI HATI KUIVAA ST LOUIS HAPO KESHO.

Image
  Mshambuliaji wa Yanga, Juma Mahadhi yuko kwenye hatihati ya kutocheza mchezo wa kesho jioni dhidi ya St. Louis kutokana na kuugua ghafla asubuhi ya leo. Mahadhi mfungaji wa bao pekee la Yanga katika mchezo wa kwanza uliofanyika Dar es Salaam alishindwa hakuhudhuria mazoezi ya asubuhi na wenzake baada ya kusumbuliwa na tatizo la mafindofindo. Baada ya kupatiwa matibabu asubuhi, Mahadhi hakuweza kufanya mazoezi na wenzake lengo likiwa ni kumpumzisha asipate madhara zaidi. Hata hivyo, mshambuliaji huyo alisema anaendelea vizuri na kuna uwezekano mkubwa akacheza kesho. "Naendelea vizuri na kama Mungu akinijalia nikiamka salama, nitakuwa fiti kucheza mechi," alisema Mahadhi

HIKI HAPA KIKOSI CHA SIMBA KITAKACHO ANZA DHIDI YA GENDARMERIE

Image
1:Aishi Manula 2:Nicholaus Gyan 3:Asante Kwasi 4:Juuko Mrishid 5:Yusuph Mlipili 6:Erasto Nyoni 7:Shiza Kichuya 8:James Kotei 9:Emmanuel Okwi 10:Mzamiru Yassin 11:Jonas Mkude Kikosi cha Akiba 1:Emmanuel Mseja 2:Mohamed Hussein 3:Mwinyi Kazimoto 4:Said Ndemla 5:Paul Bukaba 6Ally Shomary 7:Moses Kitandu

KIUNGO WA APR AIPA YANGA USHINDI

Image
By Charles Abel Shelisheli.  Kiungo wa zamani wa Azam na nahodha wa APR, Baptiste Mugiraneza ameiombea dua zuri Yanga ili kufuzu hatua inayofuata. Mugiraneza wamekutana na Yanga hapa Shelisheli kwa ajili ya mechi zao za marudiano kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho dhidi ya timu za hapa. APR  itafungua dimba kwa kucheza na Anse Reunion leo Jumanne kwenye Kombe la Shirikisho na siku inayofuata Yanga watacheza na St. Louis. Hata hivyo pamoja na Yanga kuibuka na ushindi wa bao 1-0 kwenye mechi ya kwanza, Mugiraneza anaamini watasonga mbele kwenda hatua inayofuata. "Yanga wako kwenye wakati mgumu kuliko sisi, lakini naamini watafanya vizuri kwenye mechi yao ya marudiano," alisema Mugiraneza.

BAYERN YAZIDI KUWAJALI MASHABIKI WAO.

Image
Klabu ya Bayern Munich imeingia mkataba na hoteli maarufu ya Courtyard by Marriott kutengeneza vyumba ambavyo vitawawezesha baadhi ya mashabiki wake kushuhudia mechi zake kwenye Uwanja wa Allianz Arena wakiwa kitandani. Hoteli hiyo itajenga uwanja huo ambao sehemu ya vyumba vyake vitakuwa vikiangalia sehemu ya uwanja huo. Hivyo watakaopanga, pamoja na kupata huduma ya kulala, watakuwa wakipata nafasi ya kuangalia mechi uwanjani hapo wakiwa vyumbani mwao.

Simba, Yanga Acheni Kulalamika- Mwakyembe

Image
Baada ya kumalizika kwa mchezo wa kombe la shirikisho Afrika ambao Simba SC iliibuka na ushindi wa mabao 4 – 0 dhidi ya Gendarmerie Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt Harrison Mwakyembe amesema kuwa amefurahishwa na matokeo yaliyopatikana huku akiwataka Yanga SC kuacha kulalamika na badala yake waweke akili yao zaidi katika mchezo wao wa marudiano dhidi ya St Louis. “Ni bahatika kuiyona mechi ya leo, ilikuwa nzuri sana unaiyona Simba SC kama timu ambayo kweli ilikuwa kambini na ina mwalimu na uwelewano wa hali ya juu.” “Mechi ulikuwa nzuri sana nimefurahia na kama kiwango cha mchezo wa mpira Tanzania kitakuwa hiki kama alivyosema mzee wetu Ali Hassan Mwinyi sisi siyo tena kichwa cha mwendawazimu ila cha muungwana ambacho kila mtu lazima akisogelee kwa uwangalifu mkubwa sana.” Waziri Mwakyembe alipo ulizwa kuhusu malalamiko ya Yanga SC kukosa nafasi ya kufanya mazoezi siku moja kabla ya mechi yao ya kimataifa dhidi ya St Louis amesema “Niwashauri Yanga SC kwamba aki

KIKOSI CHA YANGA KITAKACHO VAANA NA LIPULI FC LEO. Samora.

Image

YANGA KUFUATA NYAYO ZA SIMBA.

Image
Mambo yanabadilika kwa kasi kubwa na huenda itakuwa ni vigumu sana kuyazuia mabadiliko hasa katika klabu kongwe kama Yanga na Simba. Simba wameanza na watani wao, Yanga nao wanaonekana wako njiani. Kwani Kamati ya Mabadiliko ya Mfumo wa Uendeshaji wa Klabu ya Yanga chini ya mwenyekiti wake, Wakili, Alex Mgongolwa kukutana kwa ajili ya kufikia muafaka. Unaweza kusema ni neema inakaribia Yanga kwani mara baada ya kamati hiyo kukutana itapeleka ripoti kwenye Kamati ya Utendaji ya timu hiyo itakayotoa majibu kipi kifanyike. Yanga wanataka kuleta mabadiliko hayo, ikiwa ni siku chache Simba kubadili mfumo wa uendeshaji wa timu hiyo kwa kumuuzia hisa mfanyabiashara maarufu, Mohammed Dewji ‘Mo’. Taarifa zinaeleza kamati hiyo ilikutana juzi Jumatatu usiku na kujadili mfumo wa mabadiliko hayo ya Klabu ya Yanga. “Kamati yetu mpya tuliyoiteua ya Mabadiliko ya Uendeshaji wa klabu ilikutana juzi Jumatatu usiku na kikubwa ilikuwa makubaliano ya jinsi ya kuendesha klabu yetu ambayo inatu

YANGA YAINYOSHEA MIKONO TIMU YA IHEFU FC.

Image
LICHA ya mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga  kuiondosha Timu ya Ihefu FC kwenye mashindano ya kombe la shirikisho, Kocha msaidizi wa Wanajangwani hao, Shadrack Nsajigwa, amewanyooshea mikono Ihefu kutokana na kiwango walichoonyesha. Akizungumza baada ya mchezo huo kumalizika katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya, Nsajigwa alikiri vijana hao kutoka katika mabonde ya Mpunga wilayani Mbarali kuonyesha mchezo mzuri kuliko Yanga inayodhaminiwa na Kampuni ya Kubashiri Matokeo Michezoni ya SportPesa. Alisema timu hiyo iliyojaa vijana, ilicheza vizuri na kwa nguvu katika dakika zote 90 na kwamba Yanga wao walianza kuonyesha mchezo mzuri katika dakika 45 za kipindi cha pili. “Nafurahi tumepata ushindi unaotufanya tusonge mbele katika mashindano haya, lakini vijana wa Ihefu wameonyesha mchezo mzuri kuliko sisi na wamecheza kwa nguvu muda wote, penalti ni bahati na yeyote anaweza kukosa,” alisema Nsajigwa. Kwa upande wake Kocha Mkuu wa Ihefu FC, Michael Kasegeya, a