Posts

Mkojo wa Wema watikisa Mahakamani

Image
KESI inayomkabili staa wa Bongo Muvi, Wema Sepetu, jana ilichukua sura mpya baada ya mawakili wa pande mbili, ule wa utetezi na Jamhuri kuchuana kuhusu mkojo wa msanii huyo uliochukuliwa na kupimwa na Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali wakati wa upelelezi wa polisi kuhusiana na mwanadada huyo kudaiwa kutumia madawa ya kulevya.  Mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Thomas Simba, shahidi wa kwanza wa upande wa Jamhuri aliyefahamika kwa jina la Elias Mulima kutoka Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali akisoma ripoti ya uchunguzi alisema mahakamani hapo kuwa, mkojo wa Wema baada ya kupimwa ulikutwa na chembechembe za bangi.  Hata hivyo, wakili wa utetezi, Peter Kibatala, alisema ripoti hiyo iliyosomwa na Mulima ina upungufu mwingi wa kisheria. Baada ya kutokea malumbano hayo Hakimu Mkazi Simba aliwaomba mawakili wa pande zote mbili kuridhia apate muda wa kuipitia taarifa hiyo ya Ofisi ya Mkemia Mkuu ili itakapoendelea aweze kuitolea ufafanuzi. Awali, kesi hiyo iliahirishwa kusi...

Simba Yamtangaza HARUNA NIYONZIMA

Image
Uongozi wa klabu ya Simba kupitia kwa Afisa habari wake Haji Manara wamethibitisha kumsajili kiungo mwenye uraia wa Rwanda Haruna Niyonzima kuwatumuika wanamsimbazi hao.  Hayo yameweka wazi leo na Manara wakati alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari katika kumbi za mikutano za 'New Millenium Tower' eneo la Makumbusho Jijini Dar es Salaam na kusema Niyonzima ni mmoja wa wachezaji ambao watashiriki katika mchezo wao wa kwanza wa 'Simba Day' Agosti nane.  "Kuna mambo anayashughulikia huko Kigali akimaliza atakuja inaweza akaja na timu au kabla ila atacheza katika mechi ya ufunguzi Simba day. tarehe 8 kutakuwa na burudani mbalimbali ambapo U -20 ya Simba itacheza na timu ambayo itatangazwa kesho, 'maveteran' wa Simba pia  watacheza,Simba Queens watacheza) wapinzani wao pia kutajwa kesho. Pia siku hiyo kutaanzishwa zawadi kwa wachezaji bora zaidi wa msimu ambapo tutamtangaza  mchezaji wa zamani aliyechezea simba kwa mafanikio makubwa.", amesema Mana...

Dili la HIMID MAO na NGASA Kutumia yanga

Image
CLARA ALPHONCE NA SAADA SALIM BAADA ya Kamati ya Usajili ya Klabu ya Yanga kumalizana na kiungo wa Mbeya City, Rafael Daud, uongozi wa mabingwa hao wa Ligi Kuu Tanzania Bara umepanga kufanya jambo kubwa katika usajili wiki hii. Mmoja wa wachezaji ambao wanatajwa kuwa watasajiliwa na klabu hiyo wiki hii ni Himid Mao wa Azam FC, kwani Yanga wana mpango wa kufanya mazungumzo na uongozi wa Azam ili waweze kufikia mwafaka na kumsajili. Taarifa ambazo tumezi pata zinadai kuwa, Kocha Mzambia, George Lwandamina, juzi alikutana na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Hussein Nyika, na kuzungumza naye masuala ya usajili, ikiwamo  kusisitiza usajili wa Mao. Chanzo hicho kimedai kuwa, Yanga wakimalizana na Azam, Mao ataonekana uwanjani rasmi Agosti 5, mwaka huu, timu hiyo itakapomenyana na Singida United katika mchezo wa kirafiki, ambao winga wake wa zamani, Mrisho Ngassa, pia anatajwa atakuwapo. Tulipomtafuta Nyika kuzungumzia mchakato wa usajili unaoendelea, alisema wanatarajia kuongeza wachez...

Aishi Manula RASMI SIMBA

Image
Golikipa Aishi Munula ambaye alikuwa anakipiga na klabu ya Azam FC amejiunga rasmi na klabu ya Simba na kesho atakwea pipa kujiunga na klabu hiyo ambayo sasa ipo nchini Afrika Kusini kwa maandalizi za msimu ujao.  Kwa mujibu wa Haji Manara amesema kuwa klabu ya Simba imeshamalizana na mchezaji huyo na kudai ameahidi makubwa kwa mashabiki wa Msimbazi  "Golikipa wa kimataifa wa Tanzania Aishi Salum Manula kesho tarehe moja, anatarajiwa kujiunga rasmi na kambi ya klabu yetu ya Simba iliopo Eden Vale Johannesburg, nchini Afrika kusini. Manula ambaye ameshamalizana kila kitu kuhusu kujiunga na klabu yetu, na ameahidi kuwapa furaha wanachama na washabiki wetu, sambamba na kuisaidia klabu kushinda mataji itakayowania msimu huu" alisema Haji Manara  Mbali na hilo Simba kesho inatarajiwa kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya mabingwa Afrika Orlando Pirates ya nchini Afrika kusini.

Magazetini leo

Image

DOWNLOAD PERFECT KOMBO REMIX kwenye blog yetu

Image
Perfect kombo remix download hapo chini click link hii https://www.jamaaonline.com/files/download/196

MJADALA MZITO simba KUHUSU KUMVUA UKAPTENI mkude

Image
Taarifa za uongozi wa timu ya Simba pamoja na benchi la ufundi chini ya kocha mkuu Joseph Omog kumvua unahodha kiungo wake wa kutumainiwa Jonas Mkude limeendelea kuzua mjadala ambapo nahodha wa zamani wa timu hiyo, Henry Joseph amefunguka. Henry Joseph maarufu kwa jina la 'Shindika' ameongea na gazeti la Mwananchi kutokea nchini Norway ambapo alisema wazi kuwa timu hiyo imefanya jambo lisilo la kiungwana kulinganisha na kazi yake aliyoifanya ndani ya timu hiyo. Shindika alisema kiungo huyo hata kama alikuwa na makosa binafsi lakini sio sababu ya yeye kuvuliwa jumla uongozi huo badala yake ilipaswa angalau apewe unahodha msaidizi ambapo alishauzoea. "Kiukweli mimi sijafurahishwa na uamuzi uliofanywa na timu kumvua unahodha kulingana na kazi kubwa anayoifanya uwanjani lakini pia ingependeza zaidi kama wangemfanya nahodha msaidizi," alisema Shindika. Katika hatua nyingine Nahodha huyo wa zamani wa Taifa Stars mbali na kukumbushia jinsi yeye mwenyewe al...