Posts

Pacquiao kukipiga

Image
Manny Pacquiao (kushoto) akinyoosha mkono wakati wa mkutano na Waandishi wa Habari kuelekea pambano lake kutetea mkanda wake wa WBO uzito wa Welter dhidi ya Jeff Horn (kulia) mjini Brisbane, Jumapil

Tanzania VS Mauritius

Timu ya mpira wa miguu Tanzania, Taifa Stars inalizimika kupapambana kadri ya uwezo wao leo ili kushinda na kujiweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele baada ya kutoka sare ya bila kufungana dhidi ya Angola mchezo uliyochezwa Jumapili iliyopita.  Timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars, inashuka dimbani leo kutupa karata yake nyingine dhidi ya Mauritius katika michuano ya kombe la COSAFA inayoendelea nchini Afrika Kusini majira ya saa 12 jioni kwa saa za Afrika Mashariki.  Stars imekuwa na maendeleo mazuri katika kikosi chake jambo ambalo limesaidia kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Malawi katika mchezo wake wa kwanza na kuweza kuleta matumaini makubwa kwa wapenzi na mashabiki wa soka nchini.  Mpaka sasa Stars wanaongoza katika kundi lake kwa pointi nne zenye magoli mawili huku wakifuatiwa na  Angola wenye goli moja na Mauritius na Malawi  wakiendelea kufurukuta

Lowassa aripoti tena Polisi na ulinzi mbali, atakiwa kuripoti July 13

Image
Dar es Salaam.  Waziri Mkuu wa zamani na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chadema, Edward Lowassa  amewasili katika makao makuu ya Jeshi la Polisi leo (Alhamisi) kama alivyoelekezwa siku ya Jumanne wiki hii baada ya kuhojiwa kwa saa nne.  Lowassa amewasili saa 5:52 asubuhi akiwa ameambata na viongozi wengine wa Chadema akiwemo mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe huku ulinzi mkali ukiwa umewekwa katika makao makuu hayo.  Kando na hao walikuwepo watu wengine aliombatana nao, lakini walizuiliwa kuingia na askari walioimarisha ulinzi katika eneo hilo.  Askari hao pia waliwafukuza waandishi wa habari waliokuwa katika eneo hilo na kuwataka kusogea mbali ya viunga vya makao makuu hayo.  Hata hivyo, baada ya muda mfupi Lowassa aliondoka katika makao makuu hayo huku Mbowe akieleza kuwa ametakiwa kurudi Julai 13 kwa kuwa upelelezi bado haujakamilika  Lowassa alitakiwa kufika polisi leo tena kwa tuhuma za kutoa kauli ya kichochezi wakati wa futari iliyoandaliw...

TRUMP aanza vita na waislam

Image
Rais wa Marekani, Donald Trump ameweka masharti mapya ya maombi ya hati za kusafiria kwa mataifa sita ya Kiislamu na wakimbizi duniani.  Moja ya masharti hayo ni kuwa anayeomba visa lazima awe na uhusiano na mtu mwenye ushirikiano wa kibiashara na Marekani.  Nchi zinazoguswa na masharti hayo ni pamoja na Iran, Libya, Somalia, Sudan Syria na Yemen.  Ujumbe kuhusu masharti hayo umetumwa katika balozi zote za nchi hizo.  Masharti hayo mapya yameanza kutekelezwa jana na yanagusa pia mahusiano ya kifamilia kama mzazi, mkeo ama mumeo, mtoto wa kiume ama wa kike aliye Marekani.  Masharti hayo yanatolewa baada ya Mahakama Kuu nchini Marekani kusitisha  kwa muda agizo la Rais Trump  la kuzuia nchi za Kiislamu kuingia Marekani, zuio ambalo lilikosolewa

MADONGO ya Manara kwa viongozi TFF

Image
Baada ya taarifa za kukamatwa kwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF, Jamal Malinzi na Katibu Mkuu wake Mwesigwa Celestine leo mapema msemaji mkuu wa klabu ya Simba (aliyesimamishwa), Haji Manara ametoa pole kwa viongozi hao. Haji Manara amesema sisi kama wanadamu tunapitia changamoto nyingi sana hivyo ni bora tukafarajiana japo hata kwa kupeana pole pale mwenzio anavyopatwa na matatizo. Haji Manara ambaye alipigwa ‘STOP’ na TFF ya kutokujihusisha na masuala ya soka kwa mwaka mmoja kwa makosa ya kinidhamu bado anaendelea na msimamo wake wa kuitumikia klabu yake ya Simba kama kawaida kwani alilitaka Shirikisho hilo limpe barua ya kumsimamisha. Poleni Viongozi wangu wa TFF,no matter wat!!ni challenges tu ktk life, bnadaam hatufai kuombeana mabaya,hata kama huwakukutendea haki, Mungu awasimamie kutendewa HAKI @tanfootball A post shared by Haji S Manara (@hajismanara) on  Jun 28, 2017 at 1:19am 

MALINZI mahakamani

Image
JAMAL Malinzi (57), Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kufikishwa mahakamani mchana huu jijini Dar es Salaam, kujibu tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka.  Taarifa kutoka ndani ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru) zinasema, Malinzi anafikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, ambako anatarajiwa kukabiliwa na mashitaka kadhaa ya ufujaji wa fedha za shirikisho, rushwa na matumizi mabaya ya madaraka.  Mbali na Malinzi mwingine anayefikishwa mahakamani pamoja naye, ni katibu mkuu wa shirikisho hilo, Selestine Mwesigwa.  “Ndio. Rais wa TFF na katibu mkuu wake, wote wawili tunawashikilia na watafikishwa mahakamani leo kujibu tuhuma zinazowakabili,” ameeleza kiongozi mmoja mwandamizi wa Takukuru ambaye hakupenda kutajwa jina lake gazetini.  Alipoulizwa kipi hasa kilichoisukuma Takukuru kuwakamata na hatimaye kutaka kuwafikisha mahakamani Malinzi na Mwesigwa, kiongozi huyo alisema, “…hayo mengine yatafahamika mahakamani. Mimi siyo m...

VIDEO:CHADEMA WAMVAA mwinyi

Image
Baraza la Wazee wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wakiongozwa na Katibu mkuu wao Roderick Lutembeka wamelaani kauli ya Aliyoitoa Rais mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassani Mwinyi, kwamba Kama isingekuwa Katiba basi Rais Magufuli angeendelea kuwa Rais bila kikomo. Hata hivyo Wametazamisha kuwa hata kwa nchi jirani husani Rwanda mambo yalianza hivo hivo kwakupata hamasa ya watu na baadae Kagame akagoma kutoka madarakani. TAZAMA FULL VIDEO HAPO CHINI...