Posts

MANULA:Ndo basi tena simba

Image
Kipa wa Azam, Aishi Manula. WAKATI wachezaji wenzake wakitarajiwa kutambulishwa kwenye sherehe za Simba Day, kipa Aishi Manula atakosa fursa hiyo ndani ya kikosi cha Simba.  Klabu ya Simba imekuwa na kawaida ya kuandaa tamasha mara moja kila mwaka ambapo huwa ni maalum kwa kukaribisha msimu husika ikiwemo kutambulisha wachezaji wao.  Taarifa ambazo imezipata Championi Ijumaa kutoka kwa bosi mkubwa wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na klabu yake ya Azam FC ni kuwa mkataba wa Manula unamalizika rasmi Agosti 10, mwaka huu huku dirisha la usajili likitarajiwa kufungwa Agosti 6, mwaka huu.  Imeelezwa kuwa kutokana na mkataba huo kumbana kipa huyo, itakuwa ngumu kwa Simba kukamilisha mchakato wa kumsajili bila kumalizana na Azam FC kwa kuwa ili asajiliwe lazima mkataba wake ndani ya Azam uvunjwe.  “Mkataba wa Manula unatarajiwa kumalizika Agosti 10, mwaka huu, kwa maana hiyo kipa huyo hatakuwepo kwenye orodha ya wachezaji wapya watakaotambulishwa katika Simba Day....

Vituko mitandaoni:Simba na yanga

Image
Simba Yanga For simba For simba

Manara alia na taarifa za Simba kupigwa 7-0

Image
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Klabu ya Simba kwa masikitiko makubwa inakanusha taarifa potofu zinazosambaa mitandaoni na kwenye baadhi ya vyombo vya habari,kuwa imecheza mechi ya kirafiki nchini Afrika kusini,na kupoteza mchezo huo.  Uzushi huo unasema Simba imefungwa mchezo huo kwa jumla ya goli 7-0, na timu ya daraja la kwanza ya nchini humo, Royal Eagles.  Kiukweli Simba haina rekodi za hovyo kama hizo kokote inapocheza duniani,na haijawahi kufungwa na klabu yoyote idadi ya magoli kama hayo,kama zilivyo klabu nyingine nchini,hususan klabu ambayo mashabiki wake ndio wanaozusha upuuzi huo.  Dunia ya leo ni ya Teknolojia, na ingekuwa ni kweli,hakuna mtanzania ambae asingeiona hii taarifa kutoka kwenye mitandao au vyombo vya habari vya Afrika kusini.  Tunapenda Umma wa watanzania utambue kwa siku zote tulizokuwa huko,program ya benchi la ufundi, ilijikita ktk kuitengeneza miili ya wachezaji kistamina.  Wiki ijayo Timu yetu inatarajiw...

Coutinho aomba kwenda BARSELONA

Image
Bado dirisha la usajili linaendelea kushika kasika kasi na taarifa za chini chini zinadai kiungo wa Liverpool Phellipe Coutinho amemuomba kocha wake Jurgen Klopp amruhusu kwenda Barcelona.  Inafahamika kwamba Barca wanaihitaji sahihi ya Coutinho na wameshatuma ofa kwa Liverpool na wameshafanya mazungumzo na Coutinho ambaye yuko tayari kujiunga nao wakati wowote.  Taarifa nyingine za usajili ni kwamba baada ya habari kuzagaa kwamba Mbappe anakwenda Real Madrid sasa Pep Gurdiola maeingia katika mapambano na anataka kutoa kitita kikubwa zaidi kwa Monaco ili kumnasa Mbappe.  Kocha wa Chelsea Antonio Conte amesema kwa sasa Harry Kane ndiye striker anayemkubali sana nje ya Chelsea lakini hawezi kumnunua kwani ana uhakika bei yake kwa sasa itakuwa iko juu sana.  Kiungo Jack Wilshaire hataki kuondoka nje ya jiji la London na anaona kama Arsenal wataamua kumuuza ni bora wamuuze humo humo London huku West Ham ikitajwa kama sehemu ambayo anaelekea Wilshaire.  Makamu wa r...

Wanaume wanaonyanyaswa na wake zao wapewa ofa lindi

Image
Na. Ahmad Mmow, Lindi.  JAPOKUWA shirika lisilo la kiserikali la msaada wa kisheria kwa wanawake na watoto mkoani Lindi (LIWOPAC) limejikita katika kutoa msaada wa kisheria kwa wanawake na watoto. Hata hivyo limetoa wito kwa wanaume waishio mkoani humu wanaofanyiwa vitendo vya kikatili na wakezao waende wapewe msaada wa kisheria.  Wito huo umetolewa leo na mkurugenzi wa shirika hilo, Cosma Bulu, wakati wa kongomano la wasaidizi wa utoaji wa huduma za msaada wa kisheria waliopo katika halmashauri za mkoa wa Lindi, lililofanyika mjini Nachingwea. Bulu alisema ingawa shirika lake limejikita limejikita zaidi katika kuwasaidia wanawake na watoto, lakini limeona kunaumuhimu mkubwa wa kuwasaidia hata wanaume wanaofanyiwa vitendo vya kikatili na wake zao.  Huku akibainisha kuwa wanaume wanaofanyiwa vitendo vya kikatili wapo. Bali wengi wao wanaona aibu kwenda kuwashitaki wake zao. Japokuwa kisheria zilizopo zinatakiwa kutumiwa na watu wa jinsia zote. "Sisi tunafahamu kuwa wapo ...

MAGAZETINI LEO 27/07/2017

Image

AZAM FC WAWABURUZA VILIVYO WANA WA PALUHENGO

Image
AZAM FC  imeshinda mechi ya kwanza ya kujiandaa na msimu ujao wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara katika ziara yake ya Nyanda za Juu Kusini baada ya kuwachapa 4-0 wenyeji, Lipuli ya Iringa jioni ya leo Uwanja wa Samora, Iringa.  Baada ya sare ya 0-0 na Mbeya City katika mchezo wa kwanza mjini Mbeya na kipigo cha 2-0 kutoka kwa Mji Njombe FC mjini Makambako, leo Azam FC iliamua kufanya kweli kujenga heshima.  Dakika 45 za kwanza zilimalizika timu hiyo ya kocha Mromania, Aristica Cioaba anayeingia katika msimu wake wa pili Azam FC ikiwa inaongoza kwa mabao 2-0.  Beki wa kati, Yakubu Mohammed ndiye aliyefungua biashara nzuri hii leo baada ya kufunga bao la kwanza dakika ya 26 kwa kichwa akimalizia mpira wa kona ya Mghana mwenzake, winga Enock Atta Agyei.  Dakika 10 baadaye, mshambuliaji mpya, Waziri Junior aliyesajiliwa kutoka Toto Africans ya Mwanza iliyoshuka Daraja, aliifungia Azam FC la pili.  Kipindi cha pili pamoja na Lipuli inayofundishwa na Nahodha...