Posts

ZAHERA KUIVURUGA SIMBA KLABU BINGWA

Image
kwa taarifa zaidi endfelea kufuatilia habari zetu kila siku na usisahau kusoma gazeti   hili la LAJIJI

Wachezaji wa Simba waliobaki kucheza fainali Kombe la Mapinduzi

Image
Wachezaji nane wa kikosi cha kwanza waliobaki Zanzibar kuungana na wale wa kikosi cha U20 kucheza mechi ya Nusu Fainali 1-Ally Salim 2-Zana Coulibaly 3-Asante Kwasi 4-Paul Bukaba 5-Yusuph Mlipili 6-Mohamed Ibrahim 7-Abdul Seleman 8-Adam Salamba  

Kikosi cha Yanga dhidi ya Jamhuri Leo hiki hapa

Image
Kikosi cha Yanga kitakachoanza leo katika mchezo wa kombe la Mapinduzi dhidi ya Jamhuri, Uwanja wa Amaan, visiwani Zanzibar. Kikosi kitakachoanza 1. Ibrahim Hamid 2. Yassin Saleh 3. Gustafa Saimon 4. Cleofas Sospeter 5. Said Juma 6. Maka Edward 7.Shaban Mohamed 8. Pius Buswita 9. Matheo Anthony 10. Faraji Kilaza 11.Deus Kaseke Kikosi cha akiba 1. Ibrahim Abraham 2.Deonatus Mukami 3. Erick Msagati 4.Bakari Athuman 5. Cheda Hussen 6. Salum Mkama 7. Mohamed Salum 8. Ramadhan Mrisho

MGOMBEA YANGA ATOA AHADI NZITO NZITO

Image
Mgombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti katika Klabu ya Yanga Magege Chota, ameahidi kulipa fedha zote za mishahara endapo atachaguliwa. Mgombea huyo amesema kuwa Yanga hivi sasa inapitia wakati mgumu kiasi cha kwamba wachezaji wamekuwa wakicheza bila kutimiziwa stahiki zao. Chota ameeleza suala hilo litakuwa ni la kwanza kuanza kulitekeleza ili kuondoa mkanganyiko uliopo hivi sasa ndani ya kikosi ambapo kuna baadhi ya wachezaji wamekuwa wakigoma. "Unaua wachezaji wa Yanga wengi hawajalipwa fedha za mishahara yao, nawaahidi wanachama wa Yanga kuwa nitafanya zoezi la kuwalipa wachezaji ili vita ya mapambano ishike kasi endapo wakinipa kura" alisema Chota Mwanachama huyo ameanza kampeni zake rasmi baada ya hapo jana Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuthibitisha kuwa muda wa kampeni umeshaanza na utachukua siku tano

NEC yafanya uteuzi, CCM yaramba dume

Image
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeteua madiwani nane wa Viti maalum wa CCM na CHADEMA kujaza nafasi zilizoachwa wazi katika halmashauri nane za Tanzania bara, ambapo CCM yenyewe imefanikiwa kupata nafasi tano huku tatu zikienda CHADEMA. Hayo yamewekwa wazi na Mwenyekiti wa NEC, Jaji Semistocles Kaijage leo Julai 21, 2018 na kusema uteuzi huo umefanyika baada kukaa kikao cha tume hiyo cha Julai 19, 2018. Walioteuliwa ni Ajila Kalinga (CCM-Songea), Mary Kazindogo Mbilinyi (CCM Makete), Zainab Abdu Mabrouk (CCM-Kongwa), Restuta Aloyce Gardian (CCM-Muleba), Siglinda Silvester Ngwega (CCM-Morogoro). Wengine ni Zena Said Luzwilo (CCM-mji Kahama), Neema Michael Massawe (Chadema Monduli) na Teodola Muyula Kalungwana (Chadema-Iringa). "Uteuzi huu umefanyika baada ya kupokea taarifa kutoka kwa waziri mwenye dhamana ya Serikali za mitaa ambaye kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 13 cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa aliitarifu tume ya uchaguzi kuwepo kwa nafasi hizo wazi

Yanga Yaleta Kiungo Kutoka Afrika Kusini

Image
   AKILI za viongozi wa Yanga zinaonekana hazipo tena kwenye Kombe la Shirikisho inayoendelea, kwani jana wachezaji waligoma lakini kuna kiungo kutoka Afrika Kusini aliyejulikana kwa jina la Kingsley ametua kusajiliwa. Hiyo ikiwa ni siku chache tangu timu hiyo irejee nchini ikitokea Kenya ilipokwenda kucheza na Gor Mahia katika mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika Yanga walifungwa mabao 4-0. Jana wachezaji waligoma kufanya mazoezi wakishinikiza wapewe chao lakini viongozi wanaonekana kuangalia zaidi msimu ujao. Yanga tayari imesajili wachezaji sita hadi hivi sasa ambao ni Mohamed Issa ‘Banka’, Mrisho Ngassa, Deus Kaseke, Jaffary Mohamed, Heritier Makambo na Fei Toto . Kocha Mkuu wa timu hiyo Mkongoman, Mwinyi Zahera alisema kiungo huyo alitua hivi karibuni kwa siri nchini akitokea Sauzi alipokuwa akicheza soka kabla ya kukabidhiwa na kuanza majaribio. “Bado viongozi wanaendelea na usajili wao na kama unafahamu tayari nimewashauri viongozi wasajili wachezaji wengin